• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAANDISHI Ruvuma wapewa mafunzo ya ukaguzi kuchochea uwajibikaji

Imewekwa kuanzia tarehe: July 24th, 2025

Waandishi wa habari kutoka Klabu za Waandishi wa Habari Mkoa wa Ruvuma wamepatiwa mafunzo maalum ya ukaguzi yaliyolenga kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika kufuatilia matumizi ya rasilimali za umma na kuchochea uwajibikaji wa mamlaka kwa wananchi.

 Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Songea Club chini ya uratibu wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT), kupitia mpango wake wa kuimarisha ushirikiano na wadau wa habari katika shughuli za ukaguzi wa serikali.


Watoa mada wakuu katika mafunzo hayo walikuwa wataalamu wa mawasiliano kutoka NAOT akiwemo Bw. Nicolas Kilinga, Bi. Sakina Mfinanga na Bw. Focus Mauki, ambao waliwafundisha waandishi kuhusu nafasi ya vyombo vya habari katika kufuatilia utekelezaji wa mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kuandika taarifa zenye tija kwa jamii, pamoja na kushirikiana vyema na taasisi za umma katika kuhakikisha rasilimali zinatumika kwa ufanisi.

Katika mafunzo hayo, waandishi walipatiwa mbinu za kisasa za uandishi wa habari za ukaguzi, namna ya kuandaa na kuwasilisha ripoti zenye ushawishi wa kijamii, na umuhimu wa kutumia taaluma yao kama kiungo muhimu kati ya serikali na wananchi.

 “Lengo ni kuwajengea waandishi uwezo wa kufuatilia kwa makini taarifa za ukaguzi na kushinikiza utekelezaji wa mapendekezo ya CAG kwa ajili ya maendeleo ya wananchi,” alisema Bw. Mauki.

Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Ruvuma, Amon Mtega, amepongeza juhudi hizo za NAOT na kuahidi kuwa waandishi wa Ruvuma wataendelea kushirikiana na serikali kwa karibu katika kuhakikisha uwazi na uwajibikaji vinapewa kipaumbele.

 “Tunahakikisha maarifa haya tunayotumia kusaidia jamii kujua ukweli kuhusu matumizi ya fedha za umma,” alisema Mtega.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MARAIS watatu walivyoiandika historia katika kambi ya Muhukuru Songea

    July 25, 2025
  • MAMA auwa watoto watatu kwa kuwchinja Ruvuma

    July 25, 2025
  • RUVUMA kuandika historia mpya

    July 25, 2025
  • RAIS SAMIA kuzindua mradi wa uchimbaji Urani Namtumbo

    July 24, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.