• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KUELEKEA kumbukizi ya miaka 117 ya mashujaa wa vita ya Majimaji

Imewekwa kuanzia tarehe: February 19th, 2023

CHIFU WA WANGONI ALIVYOZIKWA NA WATU WAWILI WAKIWA HAI SONGEA

MOJA ya vivutio vya utalii wa kiutamaduni vinavyopatikana katika kijiji cha Mbingamharule wilaya ya Songea mkoani Ruvuma ni uwepo wa kaburi la duara ambalo Chifu Nkosi Mharule bin Zulu Gama alizikwa mwaka 1889.

 Mambo ambayo yanawashangaza wengi wanaotembelea kaburi hili ni historia inayoonesha kuwa Nkosi Mharule baada ya kufariki alizikwa kwa desturi na mila za kichifu za kabila la wangoni toka Afrika ya kusini.

 Christian Ngonyani mwenye umri wa miaka 87 ni mzee wa Mila katika kijiji cha Mbingamharule anasema kijiji hicho kimepewa jina la chifu huyo ambaye alitokea nchini Afrika ya kusini na kutawala ungoni kuanzia mwaka 1847 hadi 1889 alipofariki na kuzikwa katika kijiji hicho.

“Chifu Mharule  baada ya kufa mwaka 1889 alizikwa kwa taratibu za jadi ya machifu wa Afrika ya kusini,kaburi lake lilikuwa la mviringo,sanda yake ilikuwa ya ngozi ,alikarishwa kwenye kiti cha ngozi,walikamatwa watu wawili wakiwa hai walizikwa naye wakiwa wamesimama mbele na nyuma ya chifu’’,alisimulia mzee Ngonyani.

Amezitaja taratibu za kijadi za wakati huo zilitaka Mfalme au Chifu anapofariki ni lazima azikwe na watu wawili wakiwa hai na kusisitiza kuwa hiyo ilikuwa ni amri ya serikali ya jadi na hapakuwepo mtu aliyepinga.

 Mzee Ngonyani amewataja wengi waliokuwa wanazikwa wakiwa hai na Mfalme ni wale ambao walikuwa wamezoeana na kufanyakazi naye kwa karibu.

Hata hivyo amesema kaburi hilo linatumiwa na wananchi wa kijiji hicho kwenda kuhiji kila mwaka kwenye kaburi hilo ambalo lipo kilometa mbili toka kijijini hapo na kwamba ndugu wa Chifu Mharule toka Afrika ya Kusini huwa wanafika kufanya matambiko kwenye kaburi hilo.

Amesema mwaka juzi ukoo wa Mharule toka Afrika ya kusini walifika kushuhudia kusimikwa kwa Chifu Nkosi Imanuel Zulu Gama wa Tano ambaye ndiyo chifu wa wangoni wa sasa.

Machifu watano wa kabila la wangoni ni Nkosi Mharule Zulu Gama alifariki mwaka 1889,Nkosi Mputa Gama ambaye alinyongwa na wajerumani mwaka 1906,Nkosi Usangila Zulu Gama aliyefariki mwaka 1941,Nkosi Korofindo Zulu Gama aliyefariki Dunia mwaka 1949,Nkosi xzavery Zulu Gama alifariki mwaka 2001 na Chifu wa Wangoni wa Tano ambaye anaendelea hadi sasa ni Nkosi Emanuel Zulu Gama.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Februari 19/2023 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.