• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KUELEKEA tamasha la utamaduni la kitaifa Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: September 19th, 2024

WAMATENGO WANAVYOENDELEZA UTAMADUNI WAO KUPITIA JIWE LA MBUJI LENYE MAAJABU MENGI

MKOA wa Ruvuma una vivutio vingi tofauti ambavyo bado havitumiki katika kuchangia pato la Taifa na kuinua uchumi wa wananchi wa eneo husika.

Jiwe la Mbuji ambalo lipo katika wilaya ya Mbinga  ni miongoni mwa vivutio adimu na vya kipekee vilivyopo katika Bonde la ziwa Nyasa ambalo linajumuisha mikoa ya Mbeya,Ruvuma na Njombe.

Afisa Maliasili na Utalii wa Mkoa wa Ruvuma Africanus Challe anasema tayari Idara yake imeliingiza jiwe la Mbuji  kwenye orodha ya vivutio vya utalii katika Mkoa wa Ruvuma ili hatimaye kazi ya kutangaza eneo hilo na vivutio vingine iweze kufanyika kwa tija.

Kivutio cha jiwe la Mbuji kimekuwa gumzo kwa wengi waliosikia taarifa za kivutio hicho.Neno Mbuji kwa lugha ya kabila la wamatengo ni "Kitu kikubwa",jiwe hili lipo katika kijiji cha Mbuji kata ya Mbujii na limekuwa kivutio adimu kwa wageni wa ndani na nje ya nchi.

Jiwe la Mbuji lina maajabu mengi yakiwemo jiwe pekee kubwa Mkoani Ruvuma,Lina vyanzo vingi vya maji chini yake,ni vigumu kulipanda bila kuwaona wazee  kwa sababu ni vigumu kupanda na kulizunguka jiwe hilo bila kufuata mila na desturi za kabila la wazee wa kimatengo.

Unapofika katika jiwe hilo inakulazimu kuwatafuta wazee wanaotoa maelekezo kwa yeyote anayetaka kupanda jiwe hilo,ambalo linaheshimika sana na wakazi wanaolizunguka jiwe hilo.

Utafiti umebaini kuwa, sehemu kubwa ya wananchi wanaolizunguka jiwe jiwe la Mbuji hawajawahi kulipanda wala kulisogelea  kwa hofu ya kupoteza maisha.

Mzee Sixmund Ndunguru 100 anasema kuwa ili kupanda jiwe hilo ni lazima uwe na Mwongozaji ambaye ni mzee wa mila ambaye anazifahamu vizuri mila na taratibu za kabila la wamatengo zitakazokuwezesha kupanda jiwe hilo bila matatizo na kufurahia vivutio vilivyopo.

“Ninayafahamu maajabu ya jiwe la Mbuji tangu nikiwa na umri wa miaka mitano, mandhari ya jiwe hili hayajabadilika wala kuharibiwa Tangu nilipolifahamu jiwe hili’’, anasema Alex Ndunguru mkazi wa Mbuji.

Kulingana na Ndunguru,mimea adimu ambayo imekuwepo katika jiwe hilo tangu miaka ya 1940 alipopanda juu ya jiwe hilo kwa mara ya kwanza akiwa na baba yake mzazi na kwamba kila mtu anaruhusiwa kupanda jiwe hilo kwa kuzingatia maelekezo ya wazee wa mila na desturi.

Wamatengo wanaamini kuwa katika jiwe hilo kuna viumbe vinavyoitwa Ibuuta ambavyo ni mfano wa binadamu na kwamba viumbe hivyo ni vifupi na vya ajabu ambavyo majira ya usiku vinadaiwa kuonekana.

Hata hivyo viumbe hivyo vifupi vinapatikana katika mataifa mbalimbali ambayo yamekuwa yanapewa majina mbalimbali.

Historia inaonesha kuwa jiwe ka mbuji tangu zamani lilikuwa linatumiwa na wazee kwa ajili ya kutambika katika mila na desturi kwa kufuata mila na desturi ikiwemo kutumia unga wa mhogo na kujipaka kabla ya kuanza kupanda jiwe hilo.

Taratibu hizo sio tu zinatumika kwa ajili ya wenyeji bali hata watalii wageni wanaotaka kupanda jiwe hilo ni lazima watumie unga huo kinyume na hapo mtu anaweza kupata matatizo mengi ikiwemo kupoteza maisha.

“Iwapo mtalii ataamua kupanda jiwe hilo bila kuwaona wazee wa mila na desturi atakuwa amevunja mila na desturi na anastahili kupata adhabu.

Kutokana na maajabu hayo Ndunguru anasema ndiyo maana jiwe hilo linaitwa jiwe la maajabu  ambayo yanavutia wengi.

Uchunguzi umebaini kuwa unapoliangalia jiwe la mbuji kwa mbali linaonekana kwamba ni fupi lakini kadri unavyolikaribia ndivyo jiwe hilo linavyoonekana kuwa refu na kuwa na ugumu kulizunguka lote kwa muda mfupi hali ambayo inasababisha watalii wengi wanaotembelea jiwe hilo kuona hayo ni maajabu ambayo yanatakiwa kufanyiwa utafiti zaidi kwa kushirikiana na wazee wa mila.

Ukiliangalia jiwe hilo kwa mbali  utaona kama lina kibiongo, na kwamba jiwe hili lina sehemu maalum ya kuanzia safari ya kukwea.

Hata hivyo kinachoshangaza zaidi ufikapo hapo juu  Mwonekano wa jiwe hilo hubadilika na hapo unakuta ni kama uwanja wa michezo.

Jiwe la Mbuji pia hutumika kuwaombea watu wanaosumbuliwa na mapepo ambao hupandishwa juu ya jiwe hilo na kuombewa kimila na kwamba inaaminika mapepo hayo huondoka na wagonjwa wa mapepo wanakuwa wamepona kabisa wanaposhuka chini ya jiwe hilo.

Takwimu zinaonesha kuwa kila mwaka idadi ya watalii kutoka ndani na nje ya nchi wamekuwa wanatembelea jiwe hilo ambalo lipo umbali wa kilometa 150 kutoka makao makuu ya mkoa wa Ruvuma mjini Songea.

Leodigar Kumburu(100) mkazi wa Kijiji cha Mbuji anasema wazazi wake kabla ya kusafiri walikuwa wanakwenda kuhiji katika jiwe hilo.

Serikali ya Kijiji cha Mbuji kwa kushirikina na wazee wa mila wameamua kuboresha mazingira ya eneo la kivutio hicho cha utalii kwa kujenga nyumba za mila za wamatengo,kupika vyakula vya asili na ngoma za jadi ili watalii wakishaona jiwe hilo waweze kupata vyakula na ngoma za asili ya wamatengo hivyo wananchi kujipatia kipato.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.