• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

KUELEKEA tamasha la utamaduni Ruvuma,Nyasa ilivyosheheni vivutio mbalimbali vya utalii

Imewekwa kuanzia tarehe: September 20th, 2024

Kuelekea tamasha la utamaduni la kitaifa Ruvuma kuanzia Septemba 20 hadi 23 mwaka huu,Wilaya ya Nyasa bado ina fursa za maliasili ya kutosha zikiwemo misitu, wanyamapori, samaki, mito, ziwa, fukwe na mali kale ambazo hazijaharibiwa ndiyo maana tunasema wilaya ya Nyasa ni benki ya vivutio vya utalii na uwekezaji.

Fursa hizo zinaweza kutoa mchango mkubwa kwenye pato la Taifa na wananchi wa wilaya ya Nyasa, Mkoa wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla kupitia utalii wa kiutamaduni na ikolojia. Makao makuu ya Wilaya ya Nyasa yapo katika Mji wa Mbambabay.

Wilaya ya Nyasa ina sifa ya kuwepo kwenye bonde la ufa, ambapo bonde hilo huanza kuonekana kutoka katika maeneo ya Buruma, unaposhuka milima katika kona zinazoitwa Ambrosi.

Moja ya kivutio adimu cha utalii katika wilaya ya Nyasa ni uwepo wa Ziwa Nyasa ambalo  linapatikana Kusini – Magharibi mwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Ziwa Nyasa ni la tisa kwa ukubwa duniani,ni la tatu kwa ukubwa barani Afrika.

Ziwa hilo lina kina cha kati ya mita 426 na 758 na hii ni kutokana na kupitiwa na bonde la ufa. Kwa upande wa Tanzania mito mingi inapatikana ikitokea wilaya ya Nyasa katika safu za milima ya Livingstone, mito hiyo ni Ruhuhu, Lumeme, Ruhekei, Lwika, Mbamba Bay, Likumbo na Chiwindi ambayo huingiza maji ndani ya Ziwa Nyasa.

Ziwa Nyasa ni kuvutio kikubwa cha Utalii kanda ya kusini kwa kuwa limesheheni vitu vingi ndani yake na tabia tofauti ukilinganisha na maziwa mengine ya hapa nchini na duniani kote.

Baadhi ya tabia za ziwa hili ni uwepo wa maji meupe na maangavu eneo lote la ziwa na mawe marefu ambayo yanajulikana kwa majina ya hia na mala yanayobeba sifa tofauti.

Tabia nyingine za Ziwa hilo  ni mawimbi makubwa, fukwe nzuri na zenye sifa  tofauti,  mawe kuonekana  kama sakafu eneo la Chiwindi, fukwe zenye udongo wa mfinyanzi, kina cha maji kuwa kifupi kwa umbali

Ziwa Nyasa ni kuvutio kikubwa cha Utalii kanda ya kusini kwa kuwa limesheheni vitu vingi ndani yake na tabia tofauti ukilinganisha na maziwa mengine ya hapa nchini na duniani kote.

Baadhi ya tabia za ziwa hili ni uwepo wa maji meupe na maangavu eneo lote la ziwa na mawe marefu ambayo yanajulikana kwa majina ya hia na mala yanayobeba sifa tofauti.

Tabia nyingine za Ziwa hilo  ni mawimbi makubwa, fukwe nzuri na zenye sifa  tofauti,  mawe kuonekana  kama sakafu eneo la Chiwindi, fukwe zenye udongo wa mfinyanzi, kina cha maji kuwa kifupi kwa umbali.

Kivutio kingine ni msitu wa Mbamba ambapo wenyeji wa Wilaya ya Nyasa, hutumia msitu wa Mbamba kwa matambiko ya kupiga ngoma za kufukuza au kuita majini kwa imani zao na kwamba katika msitu huo kuna wanyama kama chui wakitokea milima ya Nangombo, Ukuli na Chinyemba ambao wanapatikana katika rasi hiyo, wakiwafuata wanyama aina ya ngedere waliopo kwa wingi katika msitu huo.

Maeneo mengine ya vivutio vya utalii kwa Wilaya hiyo anayataja kuwa ni visiwa vya Mbamba, Lundo,Hongi na jiwe la Pomonda ambapo vivutio vyote hivyo vikitangazwa vizuri vitachangia kukuza utalii kwa kuvutia watalii na wawekezaji wa ndani na nje.

Wilaya ya Nyasa pia ina vivutio vya mambokale vingi ambavyo vinapaswa kupewa kipaumbele kwa sababu vinachangia katika kukuza historia na kuendeleza utalii.

Vivutio vya mambokale vimegawanyika katika sehemu ambazo ni historia za mambokale zilizofanywa na viongozi wa nchi katika maeneo mbalimbali na kuingia kwa dini na madhehebu ambayo yameacha alama kubwa.

Baadhi ya vivutio vya mambokale katika wilaya ya Nyasa  ni Katika kijiji cha Mbamba bay wakati huo, Rais Mstaafu wa Awamu ya kwanza Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Oscar Kambona katika harakati za kudai Uhuru walilala hapo miaka ya 1956 nyumbani kwa dada wa Oscar Kambona ambapo palikuwa na ofisi ya chama cha TANU.

Magavana wa Shirikisho wa Rodesia na Nyasaland walikutana katika (Rest House) katika kijiji cha Mbambabay wakati huo,ambapo jengo ambalo hivi sasa ni ofisi ya Afisa Mtendaji wa Kata ya Mbambabay wakiwa na lengo la kuagana kutokana na vuguvugu la waafrika kudai Uhuru 1959 kushika kasi. Jengo hilo lilijengwa kwa miti.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.