• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

LIKUNGU maliasili adimu inayopatikana ziwa Nyasa pekee

Imewekwa kuanzia tarehe: April 17th, 2024


ZIWA Nyasa limezungukwa na nchi tatu ambazo ni Tanzania,Malawi na Msumbiji.Ziwa hilo lipo kwenye usawa wa meta 500 toka usawa wa bahari.

Kulingana na utafiti ambao ulifanywa na jumuiya ya nchi zilizo kusini mwa Afrika(SADC) kwa kushirikiana na  nchi ya Uingereza kwenye ziwa Nyasa,ulionesha kuwa ziwa hilo lina kiasi cha tani 165,000 za samaki.

Licha ya kuwa na samaki wa aina mbalimbali,ziwa Nyasa pia lina utajiri wa maliasili nyingine ambazo huwezi kuzipata mahali popote duniani.

Moja ya maliasili asili hizo adimu ambazo zinaweza kukuza uchumi wa watu wa Mwambao mwa ziwa Nyasa ni wadudu ambao wanafahamika kwa jina la likungu ambao wanapatikana kwenye ziwa hilo pekee.

Likungu ni kitoweo ambacho kinatajwa na wataalam wa afya kuwa na utajiri wa protini na madini mengi ya chuma kuliko vyakula vingine   hali ambayo inasababisha wananchi wanaokifahamu chakula hiki kukigombania kinapopatikana na kusababisha kuwa na soko kubwa kwa walaji.

Ukibahatika kuona  likungu  limendaliwa kuwa kitoweo huwezi kutambua kuwa hao ni wadudu mfano wa mbu ambao wametengenezwa kwa ufundi wa hali ya juu badala yake unaweza kudhani ni aina fulani ya nyama au samaki wanaopatikana ziwa Nyasa.

Efonsia Turuka(50) Mkazi wa Kijiji cha Hongi Kata ya Liuli Wilaya ya Nyasa Mkoa wa Ruvuma anasema ameanza kula likungu tangu alipokuwa ana umri wa miaka saba na kwamba kitoweo hicho ni muhimu kiuchumi na kiafya.

“Likungu ni chakula cha asili cha watu wa mwambao mwa ziwa Nyasa kinapendwa na wengi kutokana na kuwa na virutubisho adimu pia kina ladha tamu na kusababisha wengi kupenda kula ingawa upatikanaji wake ni sio wa kila siku.’’, anasisitiza Turuka.

Turuka ni mwanamke ambaye anatengeneza wadudu hao na kuwa kitoweo anasema akinamama wengi mwambao mwa ziwa Nyasa wana ujuzi wa kutengeneza wadudu hao kuwa kitoweo ambacho kinaweza kutumika kwa muda mrefu.

James Chale mkazi wa Liuli anasema wadudu kabla ya kukamatwa nchi kavu na kutengenezwa kitoweo wanaanzia kuruka angani katikati ya ziwa Nyasa kwenye mpaka wa Tanzania na nchi ya Malawi hadi kufika ufukweni mwa ziwa na kutua kwenye miti.

Challe anasema, inaaminika wadudu hao wanaotengeneza likungu wanatoka chini ya ziwa Nyasa na kuibuka juu ya ziwa wakiwa ndani ya  mfano wa puto la asili.

“Wakishaibuka juu ya ziwa puto hilo hupasuka na wadudu hao kusambaa hewani kwa mbali wanaonekana mfano wa kimbunga  ambacho kinakwenda taratibu  kulingana na kasi ya upepo hadi nchi kavu.

Anasema wanawake wakiona hali hiyo wanajiandaa kuwakamata wadudu hao ambao baada ya kufika nchi kavu wanatua kwenye majani ya miti iliyopo jirani na ziwa Nyasa.

Veronika Kamanga mkazi wa Liuli  anasema wadudu hao wakitua kwenye majani ya miti akinamama wakiwa na vifaa maalum kama vile vikapu walivyovilowanisha kwa maji wanatumia mianzi  kufunga vikapu hivyo na kuanza kuwakusanya wadudu hao ambao wanajaa kwenye vikapu hivyo na baadaye kuwafinyanga na kuwatengeneza katika maumbo tofauti yakiwemo duara au ngumi.

“Mara baada ya likungu kutengenezwa katika umbo la duara akinamama wanazungushia majani ya migomba kisha wanatumia mkaa kuanza kulichoma hadi majani ya mgomba yanapokuwa yameungua yanaashiria kuwa likungu limeiva hivyo wanatoa kwenye mkaa tayari kwa kuliwa’’,anasema.

Hata hivyo anasema likungu hilo kabla ya kuliwa kama kitoweo wakazi wa mwambao  wanaunga kwa kutumia karanga,nazi  au kuchemsha kwa maji na chumvi.

Likingu ili liweze kusafirisha maeneo ya mbali kutoka ziwa Nyasa,akinamama hao  wanaendelea kulikausha kwenye jua ili lisiweze kuharibika na kwamba likungu linaweza kukaa bila kuharibika kwa siku 30.

Likungu mwambao mwa ziwa Nyasa linauzwa kati ya shilingi 1000 hadi  2,000 kutegemeana na ukubwa wake.

Hata hivyo sio jambo rahisi kulikuta likungu sokoni kutokana na watu wengi wanaolijua kununua kwa wingi na kusababisha kuwa na uhaba mkubwa wa upatikanaji wa kitoweo hicho adimu duniani.

 

Vikta Zambia Mkazi wa Kijiji cha Nkali ziwa Nyasa anasema hadi sasa asili ya likungu  haifahamiki vizuri ingawa baadhi ya watu wanadai kuwa  ni watoto wa samaki wakubwa.

Zambia anabainisha kuwa katika ziwa Nyasa kuna samaki wakubwa wanaitwa bogobogo ambao ukubwa wa samaki hao unafanana na tumbo la mbuzi mkubwa hivyo inaaminika likungu wanakuwa ndani ya tumbo la samaki hao.

“Samaki hao wanapatikana katikati ya ziwa Nyasa ndiyo wanaowatapika wadudu hao ambao wanaruka hadi nchi kavu na kutua kwenye majani ya miti,baada ya siku tatu wasipookotwa wadudu hao baadhi yao inadaiwa wanarudi tena  hadi katikati ya ziwa na kumezwa tena na samaki hao’’,anadai Zambia.

Baadhi ya wavuvi wanaovua samaki aina bogobogo katika ziwa Nyasa akiwemo Martin Challe,John Ndomba na Frank Vumu wamekiri kuwa ukimpasua samaki huyo kwenye tumbo lake unakuta amemeza wadudu hao aina ya likungu.

Hata hivyo wanadai kuwa bado haijathibitika kisanyansi iwapo samaki hao wanaweza kuzaa wadudu kwa kuwa samaki anazaa watoto wa samaki.

Wavuvi hao wanadai kuwa siku ambayo likungu linamwagika katika ziwa Nyasa, samaki wakubwa wanaovuliwa  mbali katika ziwa Nyasa hasa aina ya bogobogo,kambale na mbufu  wanapatikana kwa wingi hali ambayo inaonesha kuwa kuna uhusiano wa  likungu na samaki wakubwa.

Anania Nkomola Mkazi wa Kijiji cha Mkili mwambao mwa ziwa Nyasa anasema likungu ni wadudu ambao wanaibuka kwa kusukumwa na upepo kutoka katikati ya ziwa Nyasa wakiwa mfano wa moshi.

Utafiti unaonesha kuwa likungu ni lishe muhimu inayotengenezwa kwa njia mbalimbali kama vile kuchomwa na kuchemshwa na kwamba unaweza kula likungu likiwa bichi.

 

Watalaam wa afya wamethibitisha likungu huongeza damu kwa  haraka  hivyo wakazi wa mwambao mwa ziwa Nyasa ambao wanashambuliwa na malaria,likungu ndiyo lishe muhimu ambayo inawasaidia kukabiliana na tatizo la upungufu wa damu.

Happy Lazaro Muuguzi Mwandamizi na mwenyeji wa Wilaya ya Nyasa Mkoa wa Ruvuma anasema mgonjwa ambaye amepungukiwa damu akitumia likungu katika kipindi cha siku saba damu inarudi katika kiwango cha kawaida.

 Anasisitiza kuwa likungu limesaidia kupunguza tatizo la watu wanaokabiliwa na upungufu wa damu  mwambao mwa ziwa Nyasa hasa kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano ambao wanashambuliwa zaidi ya ugonjwa wa malaria

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.