• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAAFISA ugani 34 Ruvuma wapata mafunzo ya upimaji wa afya ya udongo

Imewekwa kuanzia tarehe: May 20th, 2022

AFISA Elimu Mkoa wa Ruvuma Emmanuel Kisongo  amemwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Steven Ndaki kufungua mafunzo ya  maafisa ugani 34  ya maandalizi ya upimaji wa afya ya udongo .

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo Kisongo amesema wataalam wa kilimo ngazi ya Kata na vijiji mafunzo hayo yatawajengea uwezo wa kutekeleza zoezi la upimaji wa udongo litakalofanyika katika vijiji 100 ndani ya Mkoa wa Ruvuma.

Kisongo ametoa rai kwa maafisa kilimo waliopata mafunzo hayo wakasimamie na kutekeleza kwa weledi zoezi la upimaji wa afya ya udongo kwa ujumla wake hususani katika vijiji vitatu hadi vine kwa kila afisa kilimo.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametoa pikipiki 7000 kwa maafisa ugani wa Kata na Vijiji kwa nchi nzima,Mkoa wa Ruvuma  tumepata pikipiki 282”.

Amesema maafisa ugani wa Kata na Vijiji wa Mkoa wa Ruvuma kila mmoja atapata pikipiki moja na seti ya  vifaa vya kutolea huduma  za ugani katika zoezi la kutambua afya ya udongo katika maeneo mbalimbali ndani ya Mkoa.

Mtafiti Mkuu wa Udongo Kutoka TARI –UYOLE  Fredrick Mlowe katika mafunzo hayo  amesema zoezi hili lipokatika awamu ya tatu ya utekelezaji ikiwemo awamu ya kwanza ilikuwa Mkoa wa Mbeya na Songwe awamu ya pili Rukwa,Mbeya ,Iringa na Morogoro.

Mlowe amesema dhima ya mafunzo haya ni kwaajili ya kujenga uelewa  wa afya ya udongo katika kanda  na  matokokeo yake kushauli makampuni ya uzalishaji wa Mbolea na kutoa mapendekezo ya mazao mbalimbali na kurudi katika tija inayostahili.

Mtafiti wa afya ya udongo amesema matokeo hayo yatakuwa na kazi kumi kuwasaidia wazalishaji wa mbolea watengeneze mbolea inayoendana na hali ya maeneo  kulingana na matokeo yaliyopatikana katika upimaji wa afya ya udongo.

Kwa upande wake afisa biashara Mkoa wa Ruvuma Martin Joseph akimwakilisha Katubu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Jeremia Sendoro katika mafunzo hayo amesema baada ya upimaji wa afya ya udongo Mkoa utakuwa na kilimo chenye tija ikiwa Mkoa wa Ruvuma ni Mkoa wa Kilimo.

Amesema kwa maafisa ugani zoezi la mafunzo hayo ni muhimu ili wakashiriki kusaidia wakulima wa Mkoa wa Ruvuma waweze kujua matumizi sahihi ya mbolea ili waweze kulima kwa tija ikiwa mkoa wa Ruvuma kwa miaka mitatu mfululizo umeongozo kwa mazao ya chakula.

“ Nawaomba maafisa ugani kufanya kazi kwa uadilili  kwa maeneo sahihi ,Rais alipokuwa Tabora ameeleza mwaka wa fedha utakaanza julai kilimo ni kipaumbele cha kwanza “.

Amesema kilimo ili kilete tija wataalamu mnatakiwa mfanye vizuri  kwenye maeneo yote yanayohusika ikiwa kupima afya ya udongo,matumizi ya mbolea sahihi na kutoa elimu kwa wakulimu”.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Mei 20,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.