• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAAGIZO ya Waziri wa Utumishi kuhusu serikali Mtandao

Imewekwa kuanzia tarehe: February 10th, 2023

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya  Utumishi wa Umma na Utawala Bora  Mheshimiwa Jenista Mhagama  amezitaka Taasisi zote za umma  nchini kuhakikisha zinazingatia  na kufuata sheria, na kanuni za  serikali mtandao  .

Ameyasema hayo  Februari 10,2023 kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano (AICC) jijini Arusha wakati akifunga  kikao kazi cha 3 cha serikali mtandao kilichowashirikisha  zaidi ya watumishi wa umma 1600 kutoka mikoa mbalimbali nchini. 

Amesema kuwa,ni lazima taasisi zote za umma zihakikishe zinafuata sheria zilizopo ili kuwezesha kufanya kazi kwa weledi na wazalendo kwa ustawi wa nchi yetu na kuweza kuokoa gharama  kupitia huduma za kidigitali. 

“Naagiza mkaanze kufanya vikao vya kitaasisi  kila mwaka katika ngazi za wilaya na mkoa katika kuhakikisha mnatathimini huduma ya serikali mtandao katika ngazi za wilaya na mkoa ili huduma hiyo iweze kuboreshwa  na kutumia na taasisi zote za umma.”amesema  Waziri Jenista .

Aidha amewataka kupitia kikao hicho wakatekeleze  maazimio  yote  waliyojiwekea huku akiwataka kuendana na mabadiliko  ya kasi ya duniani ya teknolojia yaliyopo hivi sasa kwani hawatakiwi  kuwa nyuma .

“Wataalamu na wakuu wa idara  nawaomba sana mhakikishe  mnafanya  kazi zenu  kwa weledi na uzalendo mkubwa kwa faida ya Taifa letu, huku  mkihakikisha  kila mmoja anakuwa  mwaminifu  katika usimamizi wa  mifumo ya Tehama. “amesema Waziri Mgahama.

Kwa upande wake Mmoja wa washiriki katika mkutano huo,Katibu Tawala wa mkoa wa  Njombe ,Judica Omary amesema kuwa,kikao hicho ni cha tatu kufanyika na wameweza kujadili changamoto  mbalimbali na kuweka mikakati na  maboresho mbalimbali ikiwemo ya  kuongeza matumizi ya mtandao serikali. 

Amesema kuwa, kikao hicho kimekuwa na manufaa makubwa kwao watumiaji  wa serikali mtandao katika kukuza taaluma zao  .

Amesema kuwa,wamejiwekea mikakati ya kuhakikisha wanaenda kutekeleza huduma ya serikali mtandao katika taasisi zao kwa ajili ya kuboresha utendaji kazi wa taasisi zao.

“Kwa pamoja tumejiwekea mikakati ya kuhakikisha tunaenda kufanya vikao vyetu  kidigitali katika vikao mbalimbali ikiwemo vikao vya madiwani na kuondokana na matumizi ya makaratasi.”amesema.

Naye Mkurugenzi  wa Mamlaka ya serikali mtandao (eGA) ,Mhandisi Benedict Ndomba akielekezea maazimio waliyojiwekea amesema kuwa , kwa  pamoja wameweza kujiwekea  maazimio mbalimbali ikiwemo kuhakikisha taasisi za umma anatumia huduma ya serikali mtandao katika kuendesha shughuli zake pamoja na vikao vya madiwani ili kuweza kupunguza  matumizi ya makaratasi. 

Amesema kuwa,wamejiwekea maazimio ya kuhakikisha tovuti  zote zinaboreshwa  ili kuweza kwenda kisasa zaidi ,huku wakizitaka taasisi za umma kutoa  kipaumbele kwenye maswala ya Tehama .

Aidha amesema  kuwa,maazimio mengine ni pamoja na kuhakikisha wakuu wa taasisi za umma kuhakikisha wanasimamia kikamilifu usimamizi wa sheria za serikali mtandao, sambamba na kuiomba  serikali kuanzisha upekuzi kwa watumiaji wa huduma za Tehama. 

Kwa upande wake Naibu katibu mkuu ofisi ya Rais,menejimenti ya utumishi  wa umma na utawala  bora,Xavier  Daudi amesema kuwa, wanaenda kuyafanyia  kazi mapendekezo yote yaliyotolewa  katika kuhakikisha huduma ya serikali mtandao ina imarika zaidi. 

“Tunaendelea  kusisitiza zaidi matumizi ya Tehama kwani yatasaidia sana kuokoa gharama ya kutumia matumizi ya makaratasi huku tuhakikisha kunakuwepo  kwa matumizi  sahihi ya huduma mtandao. “amesema.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.