• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAAJABU ya Fukwe za Mhalo ziwa Nyasa,unaweza kuona mipaka ya nchi mbili kwa wakati mmoja

Imewekwa kuanzia tarehe: October 16th, 2020


Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma imebarikiwa kuwa na fukwe za asili katika ziwa Nyasa ambazo hazifanani na fukwe nyingine zozote duniani na endapo zitaendelezwa zinaweza kuwa chanzo muhimu cha mapato kwa serikali na wananchi.

Fukwe ya Mhalo iliyopo katika kijiji cha Ruhekei Kata ya Kilosa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa  imeendelezwa kwa kujengwa vivutio vya utalii pamoja na hoteli ya Mhalo beach Lodge iliyojengwa mwambao mwa fukwe za Mhalo.

Benado Lisambo ni Meneja wa Mhalo Beach Lodge  anasema fukwe hizo zina maajabu ambayo hayawezi kupatikana sehemu nyingine hali ambayo inavutia wageni wengi wa ndani na nje ya nchi kufanya utalii na kupata huduma zote zinazostahili kwa watalii.

Anakitaja kivutio kikubwa katika fukwe hizo kuwa ni mtalii anaweza kuona mipaka miwili ya nchi mbili  za Malawi na Msumbiji kwa wakati mmoja jambo ambalo linawavutia watalii wengi wanaotembelea fukwe hizo.

“Sisi wilaya Nyasa tuna bahati sana,ukiwa hapa Mhalo beach ukiangalia kusini unaona milima ya nchi ya Msumbiji na ukiangalia Magharibi unaona milima ya nchi ya Malawi,wakati wa usiku unaweza kuona taa za magari katika nchi hizo kwa kweli inavutia sana’’,anasisitiza Lisambo.

Hata hivyo anasema fukwe yote ya Mhalo inavutia wageni wengi wa ndani na nje ya nchi kwa sababu haina uchafu,maji yake ni maangavu hali ambayo inamwezesha mtalii kuwaona samaki  wanavyotembea ndani ya maji katika ziwa Nyasa.

Kulingana na Meneja huyo,toka fukwe ya Mhalo hadi mpakani na nchi ya Msumbiji ni umbali wa kilometa 30 na kwamba unaweza kusafiri kwa boti kupitia ziwa Nyasa na kwamba  kusafiri kwa boti toka fukwe ya Mhalo hadi nchini Malawi ni safari ya saa sita.

Anawataja watalii ambao wametembelea fukwe za Mhalo kuwa wametoka nchi za  Ujerumani, Italia, Uingereza, Marekani, Japan,Afrika ya Kusini,Malawi, Msumbiji, Zimbabwe na kwamba wanapokea pia watalii wengi kutoka ndani ya nchi.

“Watalii wakifika hapa Mhalo beach kuna vivutio vingi,   wanaweza kufanya utalii wa kuogelea,kupanda milima ya Livingstone, kutembea ufukweni kilometa mbili,kuona ngoma za asili mwambao mwa ziwa Nyasa,ikiwemo ngoma ya mganda,kioda na lindeku na kufanya safari za majini kwa kutumia boti’’,anasema Lisambo.

Joseph Ndomondo Mwongoza watalii Mkazi wa Liuli ziwa Nyasa anasema fukwe za ziwa Nyasa upande wa Tanzania ni bora zaidi kwa kuwa ni za asili ambazo zimetengenezwa na Mwenyezi Mungu mwenyewe.

“Fukwe za ziwa Nyasa upande wa Malawi zimetengenezwa toka kingo za milima hivyo zimechimbwa hali ambayo inadhihirisha ubora wake hauwezi kulingana na fukwe za ziwa Nyasa upande wa Tanzania’’,anasema Ndomondo.

Afisa Maliasili na Utalii wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Bugingo Bugingo anasema ziwa hilo limebarikiwa kuwa na fukwe nzuri za asili na zinazofaa kwa uwekezaji kwenye sekta ya utalii hivyo ametoa rai kwa wawekezaji kuwekeza ziwa Nyasa.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Oktoba 16,2020

 

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • MWENGE wa uhuru waingia Pers

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.