• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MADINI ya Urani kufungua utalii wa madini Mamtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: September 22nd, 2023


Wilaya ya Namtumbo imetajwa kuwa na fursa kubwa ya uwepo wa Utalii wa Madini baada ya kugundulika kuwa na kiasi kikubwa cha madini ya Urani ambapo ndiyo utakuwa na mgodi wa kwanza wa uzalishaji wa Madini hayo kwa Afrika Mashariki na miongoni mwa nchi chache zitakazo kuwa na mgodi wa urani duniani.

Hayo ameyabainisha Meneja wa Sehemu ya Jiolojia Maswi Solomon wakati akimuwakilisha Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kutoa mada kwenye Kongamano la Wadau kuhusu Fursa za Uwekezaji Wilaya ya Namtumbo lililofanyika katika ukumbi wa St. Agness-Namtumbo uliopo Wilayani humo.

"Mgodi wa kuzalisha Urani wa Mkuju ndiyo utakuwa mgodi wa kwanza Afrika Mashariki kuzalisha Urani, hivyo tunaona ni fursa kwetu katika kuchochea Utalii wa Madini kwa watu kuja kujionea ni namna gani kama nchi tumeweza kuendesha mgoni wa Urani unaoweza kutoa mionzi yenye madhara kama tahadhari isipozingatiwa, hivyo Wilaya ya Namtumbo inaenda kuwa kitovu cha Utalii wa Madini na mtapokea wageni wengi kuja kujifunza uzalishaji wa madini hayo kama ambavyo na sisi tumekuwa tukienda kujifunza kwenye migodi ya nchi kama Namibia," amesema Maswi.

Maswi amesema GST  inajukumu kubwa la kukusanya taarifa za madini kwa ajili ya kuchochea uwekezaji na kuishauri Serekali lakini pia, ina jukumu la kutoa elimu ya majanga ya asili ya Jiolojia ikiwemo matetemeko ya ardhi na madhara ya Jiolojia kama milipuko ya volkano na miamba inayoweza kuwa na sumu au mionzi.

Pia, Maswi amesema Namtumbo imebahatika kuwa na madini ya Urani ambayo yanatumika kutengeneza nishati safi isiyo na hewa ya ukaa na amewatoa wasiwasi wakazi wa Namtumbo kuwa, uchimbaji wa madini ya Urani hauwezi kuathiri mazingira kama taratibu za kitaalamu zitazingatiwa katika uchimbaji na uchakataji wake ambapo ametoa mfano kwa nchi za Namibia, Niger, Afrika Kusini na Gaboni ambapo uzalishaji wake unaendelea lakini hakuna madhara yoyote yaliyotokea hivyo Tanzania haita kuwa nchi ya kwanza kuwa na mgodi wa Urani kwa Afrika.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Ngollo Malenya amefarijika kuona Wilaya ya Namtumbo kuwa na madini ya aina mbalimbali ikiwemo urani, dhahabu, chuma, Ulanga na Vito mbalimbali ambapo Kampuni ya Mantra imejenga mgodi mdogo wa majaribio kwa ajili ya kuanza kuyavuna madini hayo.

"Kama tungepata Wawekezaji wengi, Wilaya ya Namtumbo tungekuwa mbali kimaendekeo hivyo, kupitia Kongamano hili naomba tushirikiane ili tuone ni kwa namna gani tutaweza kuinua Sekta ya Madini katika Wilaya yetu," amesema Malenya.

Kongamano hilo lililokutanisha zaidi ya washiriki 400 limebebwa na Kauli Mbiu isemayo "Mapinduzi ya Kilimo, Biashara Utalii Hifadhi ya Mwalimu Nyerere na Utalii wa Madini".

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.