• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAFUNZO ya utayari wa kukabili magonjwa ambukizi mikoa ya Ruvuma na Mtwara yaanza Tiffany Diamond

Imewekwa kuanzia tarehe: October 5th, 2020

MTAALAM kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dr. Justine Assenga  amesema  zaidi ya asilimia 60 ya magonjwa anayougua binadamu yanasababishwa na wanyama.

Dr.Assenga ameyasema hayo kwenye mafunzo ya utayari wa kukabili magonjwa ambukizi kwa timu za dharura za kukabili magonjwa kutoka mikoa hatarishi ya Ruvuma na Mtwara ambayo yanafanyika kwa siku tano kwenye ukumbi wa Hoteli ya Tiffany mjini Mtwara.

Kwa mujibu wa Mtaalam huyo kati ya asilimia hizo,asilimia 75 ya magonjwa hayo yanaambukizwa na wanyamapori na asilimia 20 kutoka wanyama wanaofugwa.

Ameyataja magonjwa sita hatarishi  ya milipuko kuwa ni kimeta,kichaa mbwa,bonde la ufa,mafua makali ya ndege,kutupa mimba na ebola na amewataja baadhi ya wanyama ambao ni hatarishi katika kusambaza magonjwa hayo kuwa ni popo na panya.

Akifungua mafunzo hayo,Mkurugenzi wa  Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Kanali  Jimmy Matamwe ameitaja dhana ya afya moja kuwa inawakutanisha wataalam na wadau kutoka sekta mbalimbali hususani sekta ya afya,mazingira,maliasili,mifugo na wanahabari kutekeleza agenda ya usalama wa afya duniani.

“Dhana ya afya moja inatumika zaidi kwa kuzingatia kuwa vimelea vingi vinavyosababisha magonjwa ya binadamu,asilimia 60 vinatoka kwa wanyamapori na mifugo,maambukizi yanatokea pale binadamu anapoingilia masikani ya wanyama hao bila tahadhari”,alisema.

Hata hivyo amesema kwa nchi za Afrika hali ni hatarishi zaidi kwa kuzingatia kuwa bara hili hususani sehemu ambazo zinakaribia mapori makubwa ya wanyama ikiwemo Kongo Basin ni kitovu cha magonjwa ya milipuko kama vile ebola na homa ya bonde la ufa na hivi sasa ni virusi vya corona.

Kanali Matamwe amesema imedhirika kuwa ushirikiano wa watalaam katika mifumo ya afya moja  hivi sasa ni agenda ya dunia nzima kwa sababu inapunguza gharama katika kushughulikia tishio la magonjwa yanayotokana na vimelea vyenye uwezo wa kutoka kwa wanyama kwenda binadamu.

Amesema Tanzania sio kisiwa hivyo kutokana na ongezeko la watu duniani,mabadiliko ya tabianchi na utandawazi umekuwa na mwingiliano mkubwa baina ya watu na wanyama katika mazingira yao na kusababisha kueneo kwa vimelea kwa haraka zaidi na kusababisha magonjwa kwa binadamu,wanyama na mimea.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la Chakula Duniani (FAO) Niwael Mtui ameyataja malengo ya kutoa mafunzo kwa timu ya afya moja ni  kuwajengea uwezo washiriki ili waweze kuzuia na kukabiliana na magonjwa ya mlipuko kabla hayajatokea.

Mafunzo ya utayari wa kukabili magonjwa ambukizi ya mlipuko kwa timu za dharura yanafadhiliwa na FAO kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo yalianza kutolewa mwaka 2018.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Oktoba 5,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.