• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAKAA ya mawe ya Ruvuma yalivyopaisha uchumi wa Tanzania

Imewekwa kuanzia tarehe: May 7th, 2025

MCHANGO wa Mkoa wa Ruvuma katika ukuaji wa uchumi wa Taifa umechomoza kwa kasi ya kuvutia, baada ya takwimu rasmi kuonyesha kuwa Pato la Taifa (GDP) katika mkoa huo limeongezeka kutoka Shilingi bilioni 2.37 mwaka 2012 hadi kufikia Shilingi bilioni 6.39 mwaka 2022 – ongezeko kubwa linalochagizwa na sekta ya madini na kilimo.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Mkoa wa Ruvuma umechangia wastani wa asilimia 10.5 ya Pato la Taifa kwa mfululizo wa miaka, hali inayoonesha kasi ya maendeleo na ongezeko la shughuli za kiuchumi katika kanda hiyo ya kusini mwa Tanzania.

Kwa upande wa sekta ya madini, makaa ya mawe ndiyo yanayoongoza katika kuimarisha uchumi wa mkoa huo. Katika mwaka wa fedha 2023/2024, serikali ilifanikiwa kuuza tani 1,356,249.84 za makaa ya mawe kutoka Ruvuma, zenye thamani ya zaidi ya Dola za Marekani milioni 144.9, kwa mujibu wa Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Alphonce Bikulamchi.

Kupitia mauzo hayo, serikali imekusanya Dola milioni 3.9 kama mrabaha na Dola 914,034.68 kupitia ada za ukaguzi, kiasi kikubwa cha fedha ambazo zinasaidia kuimarisha mapato ya ndani. Madini hayo yaliuzwa ndani ya nchi, katika nchi jirani, barani Ulaya na Asia kupitia bandari za Mtwara na Dar es Salaam.

“Takwimu hizi ni kielelezo tosha kuwa sekta ya madini mkoani Ruvuma si tu injini ya maendeleo ya mkoa huu, bali pia ni nguzo muhimu ya ustawi wa Taifa,” alisema Mhandisi Bikulamchi.

Katika kipindi cha Julai hadi Desemba 2023, Ofisi ya Madini ya Mkoa huo tayari ilikuwa imekusanya zaidi ya Shilingi bilioni 13, sawa na asilimia 64 ya lengo la mwaka ambalo ni Shilingi bilioni 41.

Uchimbaji wa makaa ya mawe ulianza rasmi mwaka 2011 na kampuni moja pekee – Tancoal Energy – lakini kufikia mwaka 2019, wawekezaji wengi walikuwa wamejitokeza, wakigeuza Ruvuma kuwa kitovu cha biashara ya makaa ya mawe nchini.

Mpaka sasa, ofisi ya Afisa Madini Mkazi Ruvuma imetoa jumla ya leseni 144 za utafutaji na uchimbaji wa madini, ikiwa ni pamoja na leseni za uchimbaji mkubwa, wa kati, na mdogo, pamoja na leseni za biashara kwa mawakala (dealers) na madalali (brokers).

Takwimu zaidi zinaonyesha kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022 hadi 2024/2025, serikali imekusanya jumla ya Shilingi bilioni 105.1 kutoka sekta ya madini pekee mkoani Ruvuma, sawa na asilimia 126 ya lengo la makusanyo.

“Huu ni uthibitisho wa ufanisi katika usimamizi wa makusanyo ya fedha zinazotokana na shughuli za madini, ikichangiwa na ongezeko la mauzo ya madini,” alisema Mhandisi Bikulamchi kwa msisitizo.

Mkoa wa Ruvuma unazidi kujiimarisha kama nguzo ya uchumi wa Taifa, ukionesha jinsi rasilimali asilia zinavyoweza kuchochea maendeleo endapo zitasimamiwa kwa weledi na uadilifu wa hali ya juu.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • BARAZA la wazee la Makumbusho ya majimaji lachagua viongozi wake

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.