• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAKABIDHIANO mwenge wa Uhuru kati ya Mkoa wa Ruvuma na Mtwara.Ruvuma yaandika historia

Imewekwa kuanzia tarehe: May 17th, 2025

Mwenge wa Uhuru 2025 mkoani Ruvuma, umepitia na kuridhia jumla ya miradi 76 ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 95.

 Taarifa hiyo imetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Bi. Mary Gasper Makondo, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed, wakati wa hafla ya makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru kati ya Mkoa wa Ruvuma na Mtwara iliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Lumesule, wilayani Nanyumbu mkoani Mtwara.

Mwenge wa Uhuru uliingia mkoani Ruvuma Mei 9 na kumaliza mbio zake Mei 16, ukipitia Halmashauri zote nane za mkoa huo kwa umbali wa kilomita 1,378.9.

Katika kipindi hicho, miradi yote 76 iliyotembelewa ilifanyiwa ukaguzi na hatimaye kupitishwa na timu ya wakimbiza mwenge kitaifa, ikiwa ni ishara ya mafanikio makubwa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja.

Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Katibu Tawala wa Mkoa huo, alikiri rasmi kupokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Bi. Mary Makondo na kuupongeza Mkoa wa Ruvuma kwa maandalizi mazuri na utekelezaji bora wa miradi.

 Akihutubia hadhara hiyo, Bi. Makondo alieleza kuwa wananchi wa Ruvuma wamefaidika mno na mbio za mwenge wa Uhuru ambazo zimewaamsha katika kushiriki kikamilifu kwenye masuala ya maendeleo na kuwaasa kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi mkuu 2025, sambamba na kauli mbiu ya mwaka huu isemayo "Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa Amani na Utulivu."

Aidha, Bi. Makondo alitumia fursa hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa mchango wake mkubwa katika kuleta maendeleo mkoani Ruvuma kupitia fedha za utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati.

 Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa barabara ya Mbinga–Mbamba Bay, upanuzi wa uwanja wa ndege wa Songea, ujenzi wa bandari ya Ndumbi (Nyasa), pamoja na upanuzi unaoendelea wa bandari ya Mbamba Bay.

 Alisema kuwa miundombinu ya elimu, afya, maji na umeme pia imeimarishwa kwa kiasi kikubwa kupitia juhudi za serikali ya awamu ya sita.

Kwa upande wake, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025, Ndg. Ismail Ali Ussi, alisisitiza kuwa ujumbe wa mwaka huu ni wito mahsusi kwa Watanzania kutunza amani na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu.

 Alifurahishwa na ushirikiano wa wananchi wa Ruvuma na kuwapongeza kwa kujitokeza kwa wingi wakati wa mbio za mwenge wa uhuru. hizo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MSIKIMBILIE hasara,serikali inakuja na bei ya neema kwa mahindi Julai

    May 31, 2025
  • WAKULIMA Namtumbo wachuma neema ya ufuta kwa teknlojia mpya ya mnada wa kidigitali

    May 31, 2025
  • RUSHWA yazidi kuporomoka na kukosa nafasi Ruvuma

    May 31, 2025
  • SERIKALI yatoa fidia ya bilioni 2.5 kupisha mradi wa umeme wa Grid Songea-Tunduru

    May 31, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.