• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAKAMU WA RAIS amuagiza RC Ruvuma kuongeza nguvu kudhibiti mifugo holela

Imewekwa kuanzia tarehe: July 21st, 2023

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Philip Mpango amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma na Kamati ya Ulinzi na Usalama kuongeza nguvu ya kudhibiti mifugo mingi inayooingizwa kiholea mkoani humo.

Dkt.Mpango ametoa agizo hilo wakati anazungumza na wananchi wa Kijiji Matomondo Halmashauri ya Songea akiwa katika ziara ya kikazi ya siku tano mkoani Ruvuma.

“Mikoa mingine tumeharibu ndiyo maana  wafugaji wengi wamehamia Ruvuma,Mhe.Mkuu wa Mkoa na Kamati yako ya Ulinzi na Usalama ongezeni nguvu kubaini na kudhibiti wanaoingiza kiholea ng’ombe wengi katika Mkoa wa Ruvuma’’,alisema.

Amesema Mkoa  wa Ruvuma ambao unaongoza kwa uzalishaji wa chakula nchini,hivi sasa umezidiwa na idadi kubwa ya mifugo inayozidi uwezo wa Mkoa hali ambayo inaathiri shughuli za kilimo.

Makamu wa Rais amewaonya  viongozi wote wanaopokea fedha kutoka kwa wafugaji na kuruhusu idadi kubwa ya mifugo kuingia katika Mkoa wa Ruvuma bila kuzingatia sheria na vibali  ambapo ameagiza vyombo vya usalama kuanza kuchukua hatua kali ili kukomesha tabia hiyo.

Amesisitiza kuwa ana taarifa za baadhi ya viongozi kwenye vijiji kupokea shilingi 100,000 kwa kila ng’ombe mmoja anayeingia mkoani Ruvuma ambapo amewataka wafugaji kuondoka kwa wakulima na  Kwenda kwenye vitalu walivyotengewa na mkoa.

Makamu wa Rais amesisitiza kulinda vyanzo vya maji na kuhakikisha miti rafiki ya mazingira inapandwa kwenye vyanzo vya maji ili viwe endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi katika mradi wa barabara ya lami ya Matomondo-Mlale yenye urefu wa kilometa 3.5 na barabara ya changarawe yenye urefu wa kilometa 19,Dkt.Mpango ametoa rai kwa madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani Pamoja na wananchi kuitunza barabara hiyo ambayo serikali imetoa shilingi bilioni nne kutekeleza mradi huo.

Amewaagiza TARURA kusimamia ubora wa barabara hiyo ili iweze kujengwa katika kiwango ili wananchi wapate barabara bora.

Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mheshimiwa Jenista Mhagama ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kujenga barabara hiyo ambapo ameiomba serikali kujenga barabara ya lami kuanzia Kijiji cha Matomondo hadi Kizuka kwa kuwa barabara hiyo ni muhimu kiuchumi na kiulinzi.

Makamu wa Rais yupo mkoani Ruvuma kwa ziara ya kikazi ya siku tano kuanzia Julai 20,2023 hadi Julai 24,2023.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.