• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAKAMU wa Rais kuanza ziara ya kikazi ya siku tano mkoani Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: July 19th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.Philipo Isdory Mpango anatarajia kuanza ziara ya kikazi  mkoani Ruvuma kuanzia Julai 20,2023 hadi Julai 24,2023.

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake mjini Songea Kanali Thomas amesema Julai 20,2023 majira ya 5.00 asubuhi Mheshimiwa Makamu wa Rais anatarajia kuwasili katika Kijiji cha Lilondo Halmashauri ya Madaba na kupokewa na viongozi wa Chama na Serikali kisha kuwasalimu wananchi.

Amesema Makamu wa Rais akiwa katika Halmashauri ya Madaba pia atasalimiana na wananchi Kijiji cha Mlilayoyo kisha kuondoka kuelekea Ikulu Ndogo mjini Songea.

“Mheshimiwa Makamu wa Rais akiwa Ikulu Ndogo Songea atapokea taarifa ya shughuli za maendeleo ya Mkoa wa Ruvuma Pamoja na kukabidhiwa taarifa ya Mkoa ya kazi za Chama Cha Mapinduzi’’,alisema.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mheshimiwa Makamu wa Rais Julai 21,2023 ataanza ziara yake katika Manispaa ya Songea ambapo atazindua kituo cha Afya Lilambo na kuwasalimia wananchi.

Amebainisha zaidi kuwa Mheshimiwa Makamu wa Rais ataondoka Lilambo na kuelekea  katika Kijiji cha Matomondo Halmashauri ya wilaya ya Songea ambako ataweka jiwe la msingi,Barabara ya kiwango cha lami ya  Matomondo hadi Mlale JKT yenye urefu wa kilometa 4.5,kisha atasalimiana na wananchi na kuelekea hospitali ya Peramiho ambako atafungua jengo la kusafishia figo na kukagua jengo la upasuaji na kusalimiana na wananchi.

Kulingana na Mkuu wa Mkoa,ziara ya Makamu wa Rais mkoani Ruvuma itaendelea Julai 22,2023 kwa Mheshimiwa Makamu wa Rais kushiriki katika kuzindua kampeni ya kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) katika uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Kampeni hiyo inatarajia kufanyika kwa siku kumi kisha kuendelea hadi Desemba 2023.Kampeni hiyo inatarajia kufanyika katika Halmashauri zote nane za Mkoa wa Ruvuma ambapo kila Halmashauri kampeni itafanyika katika kata kumi

Hata hivyo amesema baada ya uzinduzi huo Mheshimiwa Makamu wa Rais  atakwenda Kata ya Mwengemshindo Manispaa ya Songea kukagua ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa na kuzindua jengo la mionzi la hospitali ya Rufaa ya Mkoa.

Kanali Thomas amebainisha kuwa Julai 23,2023 Mheshimiwa Makamu wa Rais ataendelea na ziara yake mkoani Ruvuma kwa kutembelea wilaya za Mbinga na Nyasa na kwamba akiwa wilayani Mbinga katika Kijiji cha Kigonsera,Makamu wa Rais atasalimiana na wananchi wa Kigonsera na kisha Kwenda Mbinga mjini ambako atasalimiana na wananchi wa Mbinga mjini.

Amesema Makamu wa Rais ataondoka mjini Mbinga na kuelekea mji Mdogo wa Mbambabay wilayani Nyasa ambako anatasalimiana na wananchi kisha kuondoka na kuelekea Kijiji cha Liuli  ambako ataweka jiwe la msingi katika mradi wa maji safi Liuli na kusalimiana na wananchi wa Liuli.

“Natoa rai kwa wananchi wote kujitokeza kwa wingi katika maeneo yote ambayo Makamu wa Rais atapata fursa ya kuwasalimia wananchi’’,alisema.

Mheshimiwa Makamu wa Rais anatarajia kukamilisha ziara yake mkoani Ruvuma Jumatatu Asubuhi  Julai 24,2023.

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.