• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAKITA sekondari wamshukuru Rais Samia kuwajengea madarasa

Imewekwa kuanzia tarehe: February 8th, 2023

WANAFUNZI wa shule ya Sekondari Makita Halmashauri ya mji Mbinga mkoani Ruvuma,wameishukuru serikali kuwajengea vyumba vipya vya madarasa na kupunguza msongamano  mkubwa wa wanafunzi madarasani hivyo kuwasaidia kusoma katika mazingira mazuri.

Wamesema,wamefurahishwa na mpango wa serikali ya awamu ya sita kutokana na mkakati wake wa kuboresha na kuweka mazingira mazuri ya kujifunzia kwa wanafunzi na walimu kufundishia ikiwamo vyumba vipya vya madarasa,meza,viti na ofisi za walimu.

Pius Komba  mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule hiyo amesema,kutokana na uwekezaji huo wa serikali watahakikisha wanasoma kwa bidii na kufanya vyema katika masomo yao na hatimaye waweze kutimiza malengo yaliyowaleta shuleni.

Komba,amewaomba wazazi ambao  bado hawajapeleka watoto wao shule,kuhakikisha wanawapeleka haraka ili wakapate haki yao ya elimu kwani muda wa masomo umeshaanza na wao wamebaki nyumbani.

Aidha,amemshukuru Mkuu wa shule hiyo Mwalimu Emanuel Mwamasika kwa kukubali kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza hata wale wasiokuwa na mahitaji muhimu jambo linalowapa hamasa ya kusoma kwa bidii.

Happy Kinyunyu amesema,madarasa mapya yaliyojengwa kwa ubora yanawafanya wanafunzi  kupenda shule,kusoma kwa bidii na kuwa wasikivu darasani ikilinganishwa  na hapo awali kwa kuwa hakuna changamoto  zinazoweza kuwakatisha tamaa.

Amewaasa wanafunzi wenzake wa kike,kusoma kwa bidii ili kutimiza malengo yao badala ya kujiingiza katika ulevi,uesharati na kufanya kazi za nyumbani(House Girls) tabia iliyopelekea  baadhi ya watoto wa kike kushindwa kutumiza malengo yao.

Kwa upande wake Mkuu wa shule hiyo Emanuel Mwamasika amesema,walipokea kiasi cha Sh.milioni 40 ambazo zimefanikisha kujenga vyumba vipya viwili vya madarasa.

Amesema hapo awali kulikuwa  na uhaba mkubwa wa madarasa,lakini baada ya kupata fedha hizo na kujenga vyumba vipya sasa wanafunzi wanakaa  madarasani kwa nafasi na hakuna aliyekosa meza na kiti na wana ziada ya chumba kimoja.

Mwamasika,ameipongeza serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa kutekeleza kwa vitendo Ilani yake jambo lililosaidia kuwa na mazingira mazuri na rafiki katika sekta ya elimu hapa nchini.

Mwamasika amesema,shule hiyo imepangiwa kupokea wanafunzi 332 wa kidato cha kwanza na hadi kufikia tarehe 4 wiki iliyopita wanafunzi walioripoti ni 220 sawa na asilimia 96.4.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.