• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAKONDA atoa pole kifo cha Waziri Mkuu Mstaafu akiwa Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: February 11th, 2024

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeungana na Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Samia Suluhu Hassan kuipa pole familia ya Hayati Ngoyai Edward Lowasa na wanachama wote wa chama huku kikieleza kuwa Tanzania imepoteza kiongozi mwema ambaye ametoa mchango mkubwa katika taifa katika nafasi zote za uongozi alizohudumu.

Salamu hizo za pole zilitolewa leo na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Paul Makonda wakati akihutubia wananchi wa wilaya ya Songea Mjini mkoani Ruvuma ukiwa ni muendelezo wa ziara yake ya mikoa 20.

“Mpendwa, kiongozi wetu, na mwanachama wetu wa Chama cha Mapinduzi aliyekuwa Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Lowassa amefariki leo Februari 10 saa nane mchana katika hospitali ya Moyo pale Muhimbili,”

“Chama cha Mapinduzi kiunaungana na Mwenyekiti wetu na Watanzania wote, kuipa pole familia ya Hayati Ngoyai Edward Lowassa na wanachama wa Chama cha Mapinduzi na kumuomba Mungu kwa kudra zake atupe uvumilivu katika wakati huu mgumu wa msiba ambao wanachama wa Chama cha Mapinduzi kwa kumpoteza mwanachama na familia kumpoteza baba, mjomba na babu” Amesema Makonda.

Amesema kwa niaba ya CCM wanatoa pole kwa wanachama na wapenzi wa chama hicho,wakereketwa na Watanzania wote kwa ujumla kwa kuwa Lowasa alikuwa kiongozi mwema na kwa nafasi zake zote alitoa mchango mkubwa katika taifa hili.

Makonda amesema Hayati Lowassa atakumbukwa kwa mambo mengi lakini pia kwa umahiri wake wa kujenga hoja katika nyakati tofauti na kufanya kazi katika taifa hili lakini kwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu hawana budi kukubaliana na kazi ya Mungu.

Amesema wakati anaanza ziara yake alifanikiwa kupita katika Jimbo la Monduli na kuongelea mema yake kwasababu wote walikuwa kwenye Chama hicho.

“Wakati tunaanza ziara yetu, Dar es Salaam, tukaenda Pwani, tukaenda Tanga, Kilimanjaro, na tulipofika Arusha tulipata nafasi ya kwenda kwenye Jimbo la Monduli, kaka yangu Fredy Lowasa akiwa ndiyo Mbunge, na tulimkumbuka Mzee wetu kwasababu wote tumekuwa kwenye chama hiki na katika utumishi wa serikali tukiwafahamu viongozi wetu, Hatukujua ya kwamba kabla ya kumaliza ziara yetu tutapata taarifa nzito na ngumu kama hizi lakini yote ni mapenzi ya Mungu,”amesema.

Amesema kutokana na Rais Samia kutangaza maombolezo na kushusha bendera nusu mlingoti kwa siku tano, wao kama Chama wanajipanga kusubiri utaratibu ili wanachama wote waweze kujulishana namna watakavyoshiriki katika kumuhifadhi katika nyumba yake ya milele.

“Mheshimiwa Rais ametangaza maombolezo na kushusha bendera kwa siku tano, kupitia tangazo hilo la kiongozi wetu na Mwenyekiti wetu wa chama, na sisi kama chama tutajipanga kusubiri utaratibu ili wanachama wote tuweze kujulishana hatua na namna tutakavyoshiriki katika kumuhifadhi katika nyumba yake ya milele, mengi tutayapa na mengi tutayasema kadri ya ratiba na viongozi wetu Wakuu wanavyotuelekeze” Amesema.

Hayati Waziri Mkuu mstaafu, Lowassa amefariki Jana saa nane mchana wakati akupatiwa matibabu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Mrisho Kikwete (JKCI).

Lowassa alihudumu kama Waziri Mkuu wa Tanzania chini ya Rais wa awamu ya nne ya Rais mstaafu, Jakaya Kikwete kwa miaka mitatu, toka 2005 mpaka 2008.

Lowassa alizaliwa Agosti 26, 1953 na amefariki akiwa na umri wa miaka 70

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.