• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MALORI 120 hubeba makaa ya mawe kwa siku katika mgodi wa JITEGEMEE Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: August 19th, 2024

Meneja Uchimbaji wa kampuni ya Mgodi wa Makaa ya Mawe ya JITEGEMEE Wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma Bosco Mabena amesema malori zaidi ya 120 hubeba makaa ya mawe kwa siku katika mgodi huo na kwamba uzalishaji wa madini hayo unafanyika kwa njia za kisasa.

Mabena amesema hayo wakati anatoa taarifa ya uchimbaji madini ya makaa ya mawe kwa viongozi kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) ambao wapo mkoani Ruvuma kwenye kampeni ya kuhamasisha uwekezaji wa ndani na usajiri wa biashara TIC.

Amesema makaa ya mawe yanayozalishwa kwenye mgodi wa Kampuni ya JITEGEMEE hutumika katika viwanda vilivyopo ndani ya nchi,Afrika Mashariki na nchi za Ulaya na China.

“Huu ni mgodi wa kitanzania ambao unaendeshwa na wazawa kwa asilimia 100,tunavyo vitalu vya makaa ya mawe ambavyo vinachimba makaa ya mawe kwa njia ya kisasa kwa sababu tuna vifaa vya kisasa vikiwemo  maabara ya kisasa na mitambo ya kuchakata makaa ya mawe kwa ubora wa hali ya juu’’,alisisitiza Mabena.

Amesema makaa ya mawe yanatumika katika viwanda mbalimbali vikiwemo vya saruji katika mikoa mbalimbali nchini,pia amesema makaa ya mawe yanatumika katika viwanda vya tires,nondo na viwanda vyote vidogo vidogo vikiwemo viwanda vya nguo ambapo amesema wanapakia makaa ya mawe bandari ya nchi kavu zaidi ya 120 kwa siku.

Hata hivyo amesema Kampuni ya JITEGEMEE ina ghala la kutunzia makaa ya mawe katika bandari ya Mtwara lenye uwezo wa kutunza makaa ya mawe zaidi ya tani laki tano kwa ajili ya kuuza katika masoko ya nje ya nchi kupitia bandari ya Mtwara.

Kwa upande wake  Meneja Uhamasishaji Uwekezaji wa Ndani Kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Felix John ameipongeza Kampuni ya JITEGEMEE kwa uwekezaji mkubwa ambapo amesema TIC imefika mkoani Ruvuma  kwa lengo la kutembelea miradi ya uwekezaji  wa wazawa katika Mkoa wa Ruvuma iliyosajiriwa kupitia TIC.

Amesema TIC ipo mkoani Ruvuma kwa lengo la kutoa elimu ya uwekezaji wa ndani na usajiri wa miradi katika kituo cha TIC ambapo amesisitiza kuwa wanaamini wananchi wa Mkoa wa Ruvuma watajitokeza kwa wingi kusajiri miradi yao  ili waweze kunufaika na vivutio vya kikodi na visivyo vya kikodi vinavyotolewa na serikali kupitia TIC.

Kwa upande wake Afisa Biashara wa Mkoa wa Ruvuma Joseph Kabaro amesema bado Mkoa una fursa nyingi za uwekezaji katika sekta ya madini kwa kuwa Mkoa wa Ruvuma umebarikiwa kuwa na aina mbalimbali za madini.

Ameyataja madini hayo kuwa ni makaa ya mawe,dhahabu,chuma,uranium,madini ya vito, shaba na madini ya ujenzi ambapo amesema hadi sasa kampuni zilizojitokeza kuchumba makaa ya mawe ni 18.

Madini ya Makaa ya mawe katika Mkoa wa Ruvuma yanachimbwa katika wilaya za Songea,Mbinga,Nyasa na Namtumbo.

Kituo cha Uwekezaji Tanzania katika Mkoa  wa Ruvuma kimeweza kuwatembelea wawekezaji wazawa wawili ambao ni Kampuni ya SUPEFEO ya mjini Songea na Kampuni ya Uchimbaji madini ya JITEGEMEE wilayani Mbinga.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.