• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAMA auwa watoto watatu kwa kuwchinja Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: July 25th, 2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Ruvuma linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za mauaji ya kikatili yaliyogubika Wilaya za Namtumbo na Mbinga, likiwemo tukio la kusikitisha la mama mmoja kuwaua watoto watatu kwa kuwachinja shingoni kwa kutumia kitu chenye ncha kali, tukio linalodaiwa kuchochewa na wivu wa mapenzi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 25, 2025, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Marco Chilya, amesema tukio la kwanza lililotikisa jamii lilitokea Julai 12, 2025 majira ya saa 8 mchana katika Kijiji cha Milonji, Kata ya Lusewa, Wilaya ya Namtumbo ambapo mwanamke aitwaye Wende Luchagula (30), mkazi wa kijiji hicho, alituhumiwa kuwaua watoto wa mke mwenzake kwa kuwachinja shingoni.

Kamanda Chilya alieleza kuwa watoto waliouawa ni Lugola Samweli (6), na mapacha wawili, Kulwa Samweli na Doto Samweli, wote wa umri wa miezi 8. Alisema inadaiwa kuwa mtuhumiwa, akiwa na wivu wa mapenzi baada ya kugundua mume wake anampendelea zaidi mke mdogo na watoto wake, alisubiri mpaka mume wake na mke huyo mdogo walipoenda mnadani ndipo akatekeleza mauaji hayo ya kikatili dhidi ya watoto hao wasio na hatia.

Kwa mujibu wa Kamanda Chilya, uchunguzi wa awali umebaini kuwa mtuhumiwa alitumia kisu kuwachinja watoto hao katika mazingira ya kutisha. Miili ya marehemu ilikabidhiwa kwa familia kwa ajili ya maziko, huku mtuhumiwa akiwa mikononi mwa Polisi kwa hatua zaidi za kisheria.

Katika tukio jingine lililotokea Julai 17, 2025 majira ya saa 2 asubuhi katika Kijiji cha Lihale, Kata ya Mkako, Wilaya ya Mbinga, mkazi wa kijiji hicho, Adam Mkinga Chengula (68), aliuawa kikatili na ndugu zake wawili kwa kile kinachodaiwa kuwa ni imani za kishirikina. Kamanda Chilya amesema marehemu alikutwa ameuawa ndani ya zizi la mbuzi nyumbani kwake baada ya kunaswa na kunyongwa na ndugu zake waliotajwa kuwa ni Dastan Mkinga, mkazi wa Bombambili Songea Mjini na Leyson Mkinga, mkazi wa Ruhuwiko Songea Mjini.

Kamanda amesema baada ya tukio hilo, Jeshi la Polisi lilianzisha msako mkali na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa Leyson Mkinga Julai 24, 2025 katika eneo la Ruhuwiko, huku juhudi za kumtia nguvuni mtuhumiwa wa pili, Dastan Mkinga, zikiendelea kwa kasi.

Katika hatua nyingine, Kamanda Chilya ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa wanandoa wanaoridhia kuishi kwenye ndoa za wake zaidi ya mmoja kuhakikisha wanajenga moyo wa uvumilivu, maelewano na kuacha wivu wa mapenzi wa kupindukia. “Endapo kutatokea migogoro ya kindoa, ni busara kutafuta suluhisho kwa njia ya amani kwa kushirikisha viongozi wa dini, wazee au wataalamu wa ushauri wa ndoa,” amesema.

Matukio haya mawili ya mauaji si tu yamezua taharuki kwa wakazi wa Ruvuma, bali pia yameibua mjadala mpana kuhusu athari za wivu wa mapenzi na imani potofu katika jamii. Jeshi la Polisi limeahidi kuendelea na msako wa watuhumiwa waliobaki na kuhakikisha haki inapatikana kwa wahanga wote wa matukio haya.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MARAIS watatu walivyoiandika historia katika kambi ya Muhukuru Songea

    July 25, 2025
  • MAMA auwa watoto watatu kwa kuwchinja Ruvuma

    July 25, 2025
  • RUVUMA kuandika historia mpya

    July 25, 2025
  • RAIS SAMIA kuzindua mradi wa uchimbaji Urani Namtumbo

    July 24, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.