• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MBAUWASA yazinduliwa kwa kishindo Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: July 26th, 2025

 "Mamlaka isipojiendesha, haitakuwa na nafasi ya kuendelea – sitakubali ifutwe mikononi mwangu!" — DC Peres Magiri

Katika tukio la kihistoria linaloashiria mwanzo mpya wa huduma bora za maji safi na usafi wa mazingira, Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mheshimiwa Peres Magiri amezindua rasmi Bodi ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Wilaya ya Nyasa (MBAUWASA). Uzinduzi huo umeambatana na ugawaji wa Sheria Na.5 ya Maji ya mwaka 2019 pamoja na vitendea kazi muhimu kwa wajumbe wa bodi, ikiwa ni ishara ya dhamira thabiti ya Serikali kusogeza huduma karibu na wananchi.

Akizungumza kwa msisitizo na uzito wa kipekee, DC Magiri ametoa mwongozo mkali wa kiuongozi kwa wajumbe wa MBAUWASA, akiwataka kuwa wazalendo, wabunifu, na wenye maono ya mbali ili mamlaka hiyo ijisimamie kwa ufanisi. Alionya kuwa mamlaka isipojiendesha kitaasisi na kifedha, ipo hatarini kufutwa, jambo ambalo hatakubali litokee wakati akiwa kiongozi wa Wilaya hiyo kwa niaba ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mkurugenzi Mtendaji wa MBAUWASA Mhandisi John Guseseka amesema kuwa mamlaka hiyo ilianzishwa rasmi mwaka 2018, ikiwa katika daraja C, na eneo lake la huduma likiwa Kata za Mbamba-Bay, Kilosa, na Mtipwili. Huduma zake zimekuwa zikiwezeshwa na mapato ya ndani pamoja na uwekezaji wa Serikali Kuu katika miundombinu ya maji.

Kwa sasa, Bodi mpya iliyoteuliwa na Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso mnamo Februari 12, 2025, inatarajiwa kudumu hadi Februari 11, 2028, ikiweka kipaumbele katika huduma endelevu za maji kwa wananchi.

Wajumbe wa Bodi ya MBAUWASA

  • Stanley Vumu – Mwenyekiti

  • Asifiwe Salum – Mwakilishi wa watumiaji wa kawaida

  • Dkt. John Papalika – Wawakilishi wa wafanyabiashara

  • Veronica Simba – Mwakilishi wa wanawake

  • Leslie Kadambe – Mwakilishi wa watumiaji wakubwa

  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa na Mkurugenzi wa MBAUWASA – Kwa nyadhifa

 Kauli Mbalimbali Zenye Uzito

 “Tunataka kuongeza upatikanaji wa maji kutoka asilimia 68 hadi 85.” — Stanley Vumu, Mwenyekiti MBAUWASA
 “Viongozi wa vijiji na vitongoji simamieni elimu ya ulipiaji huduma za maji, msiwe vikwazo.” — Acheni Mwinshehe, Katibu wa CCM Wilaya ya Nyasa

Katika hotuba yake, DC Magiri hakusahau kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, akisisitiza umuhimu wa kumpa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kura za kishindo kwa kazi kubwa ya maendeleo anayoifanya, hususan katika Wilaya ya Nyasa ambako miradi mingi ya kimkakati imetekelezwa.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • HISTORIA mpya kuandikwa Namtumbo Julai 30,2025

    July 26, 2025
  • MBAUWASA yazinduliwa kwa kishindo Nyasa

    July 26, 2025
  • SONGEA yaandika ukurasa mpya wa mapinduzi ya lishe kwa watoto

    July 26, 2025
  • MARAIS watatu walivyoiandika historia katika kambi ya Muhukuru Songea

    July 25, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.