• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MBINGA kujenga shule mpya ya bweni kwa ajili ya wenye ulemavu

Imewekwa kuanzia tarehe: April 19th, 2021

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma inatarajia kujenga shule maalumu ya bweni itakayohudumia watoto wenye ulemavu na wanaohitaji uangalizi maalumu.

Akizungumza kwenye kikao cha kujadilia changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Juma Mnwele,amesema shule hiyo inayokusudia kuhudumia watoto wote wenye mahitaji maalumu na itajengwa katika Kata ya Maguu.

Amesema ujenzi wa shule hiyo unatarajia kugharimu shilingi Milioni 250 katika kwa awamu na kwamba kuanzia Julai Mosi mwaka huu Halmashauri hiyo inatarajia kutumia shilingi Milioni 100 ambazo tayari zimetengwa kwenye mpango wa bajeti wa mwaka 2021/2022  kwa ajili ya  kujenga madarasa mawili, vyoo na bweni katika shule hiyo.

“katika kuhakikisha azma ya kujenga shule hiyo inatimia, tayari Ofisi yangu imepanga ziara ya wajumbe wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ambao watatembelea Kata ya Maguu na kukagua eneo la ujenzi wa shule hiyo kabla ya mwisho wa mwezi huu’’,alisema.

Kwa upande wake Afisa Elimu Maalumu katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Happy Mpete amesema serikali imekua ikichukua jitihada mbalimbali kusaidia jamii ya watoto wenye ulemavu .

Amezitaja jitihada hizo kuwa ni kuajiri walimu wenye elimu maalumu,kujenga miundombinu rafiki kwa wenye mahitaji maalumu na kuweka vitengo maalumu kwa watoto wenye ulemavu hususani wasioona,viziwi na  watoto wenye ulemavu wa akili.

Mgeni rasmi kwenye kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Cosmas Nshenye amesema serikali inakusudia kufanya utambuzi wa watu wenye ulemavu kuanzia ngazi ya chini utakaokuza na kuongeza takwimu za uandikishaji wa shule kwa watoto wenye ulemavu.

Hata hivyo amesema uandikishaji kwa wenye ulemavu unahitaji ushirikiano na uwajibikaji wa pamoja baina ya familia, jamii na serikali na kwamba wajibu wa kwanza unaanza ngazi ya familia.

Kujengwa kwa shule hiyo kutaifanya wilaya ya Mbinga kuwa na shule  tatu maalumu, Shule mbili za awali  ni Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mbinga Girls na Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Mbinga Boys.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Aprili 18,2021

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.