• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MBINGA MJI yatumia zaidi ya bilioni tatu kujenga jengo la Halmashauri na nyumba saba za watumishi

Imewekwa kuanzia tarehe: October 17th, 2020

HALMASHAURI ya Mji wa Mbinga Mkoani Ruvuma, imetumia zaidi ya shilingi bilioni tatu zilizotolewa na serikali kwa ajili ya kutekeleza mradi wa jengo la ofisi ya Halmashauri ya Mji na nyumba saba za wakuu wa Idara.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Grace Quintine  amesema Halmashauri yake katika kipindi cha mwaka 2019/2020 ilipokea kiasi cha sh.milioni 350 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba saba za wakuu wa Idara ambazo ujenzi wake umekamilika.

“Mradi huu wa nyumba za watumishi utasaidia sana wakuu wa Idara,badala ya Halmashauri kuwalipia pango la nyumba,tutakuwa tumewasaidia nyumba hizi,mradi umefanyika kwa force account na Msimamizi Mkuu wa mradi  alikuwa ni TARURA’’,alisema Quintine.

Amesema serikali ya Awamu ya Tano pia imetoa zaidi ya shilingi bilioni 2.9  ambazo zimetumika kutekeleza mradi wa jengo la Halmashauri ya Mji wa Mbinga ambalo limeanza kutumika hivyo kuboresha mazingira ya kufanyia kazi kwa watumishi na wananchi. 

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme kwa niaba ya wananchi wa Mbinga,amemshukuru Rais Dkt John Magufuli kwa kuruhusu kiasi hicho cha mabilioni ya fedha yaliyowezesha kujengwa jengo bora la Halmashauri ya Mji wa Mbinga na nyumba saba za watumishi.

“Tuna kila sababu ya kumshukuru Rais wetu kwa zawadi hii kubwa,kwa niaba ya serikali nawapongeza wana Mbinga Mji kwa kupata jengo hili zuri na rafiki la kutolea huduma’’,alisisitiza Mndeme.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Oktoba 16,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • MWENGE wa uhuru waingia Pers

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.