• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MBINGA wajenga kituo cha afya Matiri kwa kutumia mapato ya ndani

Imewekwa kuanzia tarehe: February 14th, 2023

HALMASHAURI ya wilaya Mbinga mkoani Ruvuma,imetumia Sh.milioni 500 kutoka mapato ya ndani kujenga kituo cha afya Matiri kata ya Matiri ikiwa ni utekelezaji wa mkakati wake wa kusogeza  na kuimarisha huduma za afya kwa jamii.

Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo George Mhina amesema,fedha hizo zimetumika kwa ajili ya kujenga majengo matano ambayo ni jengo la wagonjwa wa nje(OPD)maabara,jengo la wazazi, jengo la kufulia na kichomea taka ambalo ujenzi wake utaanza hivi karibuni.

Amesema,ujenzi wa majengo hayo umekamilika kwa asilimia zaidi ya 90 na Halmashauri imepanga kuanza kutoa huduma angalau za awali mapema mwezi April.

Mhina amesema,kwa sasa kazi inayofanyika ni kutambua watumishi watakaokwenda kufanya kazi katika kituo hicho,kuleta madawa na vifaa tiba pamoja na usajili wake.


Amesema,Halmashauri  ya wilaya Mbinga kupitia mapato yake ya ndani imejipanga kuhakikisha vijiji na kata zote kuna vituo vya kisasa vya kutolea huduma ili wananchi ambao ndiyo wanufaika wanafurahia na kwenda kwenye vituo vya serikali kupata huduma mbalimbali za matibabu.

Mkazi wa kijiji cha Matiri Joseph Ndunguru amesema, kujengwa kwa kituo hicho cha afya ni ukombozi mkubwa kwao kwani  sasa wanategemea zahanati ndogo ambayo kutokana na idadi ya watu waliopo inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwamo  baadhi ya dawa,vifaa tiba na watumishi.

Nduguru ameiomba serikali,kupeleka vifaa ili ujenzi  ukamilike haraka na waweze kupata huduma zote za matibabu karibu, badala ya kuendelea kufuata baadhi ya huduma Hospitali ya wilaya Mbinga  kilomita 50 na Hospitali ya St Joseph Peramiho iliyopo umbali wa km 100.

Kwa upande wake fundi anayejenga kituo cha afya Matiri Juma Kombo amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zinazotumika kujenga na kuimarisha huduma za afya nchini.

Kombo,amewaasa mafundi wenzake wanaopata kazi za kujenga miradi mbalimbali ya maendeleo kuwa waaminifu wa fedha zinazotolewa na serikali ili iendelee kuwaamini mafundi wazawa katika ujenzi wa miradi ya maendeleo nchini.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.