• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MBINGA yafungua milango ya uwekezaji

Imewekwa kuanzia tarehe: April 22nd, 2021

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imeweka wazi milango ya uwekezaji kwa kutangaza fursa mbalimbali za kiuchumi zinazopatikana na kukaribisha watanzania kuchangamkia haraka fursa hizo kwa kuwekeza ndani ya Halmashauri hiyo.

Hayo yabebainishwa wakati wa kikao cha Baraza la Biashara la Wilaya kilichofanyika Mbinga Mjini Aprili 17, ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Juma Mnwele amesema Halmashauri hiyo ina utajiri wa fursa za kiuchumi na kutoa rai kwa mtu yeyote mwenye nia na dhamira ya kuwekeza basi kufanya hima kuja kuwekeza Mbinga.

Mkurugenzi huyo Mtendaji amebainisha kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ina maeneo mengi ya wazi, makubwa na mazuri ya uwekezaji kwa kufanyika shughuli na fursa mbalimbali kama Viwanda vya kusindika unga wenye virutubisho (Unga Lishe), vituo vya kuuzia mafuta (Petrol Stations), uchimbaji wa makaa ya mawe, uwekezaji kwenye kilimo cha mazao mbalimbali ya biashara kama parachichi, korosho, alizeti, soya, ufuta, na mengineyo ambayo kulingana na tafiti za hali ya udongo yanaelezwa kustawi vizuri kwenye maeneo mengi ndani ya Halmashauri hiyo.

Amesema anakaribisha na kuhamasisha wawekezaji kuja kwa wingi kuwekeza ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kwani Halmashauri hiyo imeweka mazingira yote rafiki na salama kwa uwekezaji ikiwemo kurahisisha upatikanaji wa ardhi na maeneo ya uwekezaji pamoja na uwepo wa miundombinu na huduma muhimu kama umeme, maji na barabara huku akitolea mfano eneo la Kiamili na miji mingine midogo ya Maguu, Matiri, Kigonsera, Ruanda na Mkako ambayo tayari yameshapimwa na kutengwa maeneo maalumu kwa ajili ya uwekezaji.

Akizungumzia kuhusu fursa za uwekezaji zilizopo Kiamili, ambako ni Makao Makuu ya Halmashauri, Mkurugenzi Mnwele amesema kwa sasa Halmashauri hiyo inatekeleza mradi wa ujenzi wa jengo la Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji na ujenzi wa stendi ya mabasi na kwamba anatoa hamasa na kuwakaribisha wadau wa uwekezaji kuchangamkia fursa zilizopo ndani ya eneo hilo, akitolea mfano kuwekeza kwenye ujenzi wa vibanda zaidi ya 200 vya biashara vitakavyojengwa kuzunguka eneo la stendi kwa kuingia ubia na Halmashauri hiyo.  

Kikao cha Baraza la Biashara Wilayani Mbinga kimefanyika na kuongozwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Mhe. Cosmas Nshenye na kuhudhuriwa na viongozi, wafanya biashara na wadau wa biashara kutoka Halmashauri zote mbili za Wilaya ya Mbinga ambazo ni Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga na Halmashauri ya Mji wa Mbinga.

   

Imeandikwa na Salum Said

Afisa Habari Mbinga

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.