• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MBUNGE azungumzia umuhimu wa sensa ya watu na makazi 2022

Imewekwa kuanzia tarehe: February 21st, 2022

MBUNGE wa Jimbo la Tunduru Kaskazini Mkoani Ruvuma Hassan Kungu,amewataka viongozi wa Dini wilayani humo,kushirikiana na serikali kuwa elimisha waumini wao kujiandaa kushiriki kuhesabiwa katika zoezi la sensa ya watu na makazi itakayofanyika Mwezi Agosti mwaka huu.

Kungu alisema  wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Nampungu kata ya Nampungu akiwa katika ziara ya kukagua na kuhimiza shughuli mbalimbali za maendeleo zinazofanywa na wananchi kwa kushirikiana na Serikali.

Alisema, kuna umuhimu mkubwa kwa viongozi wa Dini kushiriki katika zoezi hilo kwa kuhamasisha wananchi kushiriki vyema kuhesabiwa kwani wanakutana na kuongea na wananchi wengi mara kwa mara ikilinganisha na viongozi Serikali.

Alisema,sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 wilaya hiyo haikufanya vizuri kutokana na baadhi ya viongozi wa dini kupitia nyumba za ibada kuwaeleza waumini wao wasishiriki zoezi hilo kutokana na sababu zao, hivyo serikali ilishindwa kupata taarifa sahihi ya idadi ya watu waliopo.

Kwa mujibu wake,changamoto hiyo kwa kiasi kikubwa imesababisha wilaya ya Tunduru kutopata Halmashauri nyingine, licha ya kuwa na eneo kubwa na watu wengi ikilinganisha na mkoa jirani wa Mtwara.

Kungu,amewahimiza viongozi wa serikali katika ngazi mbalimbali kuhakikisha wanaelimisha wananchi umuhimu wa kushiriki katika sensa, kwa kutoa taarifa muhimu za kaya zao kwani itasaidia Serikali kuwa na taarifa sahihi na kupanga mambo mbalimbali ya mendeleo.


Aidha,amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa makarani watakaopita kwenye makazi yao kuwahesabu kwa kutoa takwimu sahihi na kuepuka kuficha baadhi ya taarifa muhimu kama idadi ya watu na mifugo.

“Ndugu zangu mwakani nchi yetu inatarajia kufanya zoezi la sensa ya watu na makazi,nawaombeni sana sana tushiriki kikamilifu kwa kutoa taarifa sahihi za kaya zetu,sisi Tunduru hatukufanya vizuri katika zoezi la sensa ya watu na makazi iliyopita,serikali haiwezi kuleta maendeleo mahali ambako hakuna taarifa na idadi sahihi ya watu, sasa hivi tunapambana kupata Halmashauri ya pili,lakini haiwezi kutupatia kama idadi ya watu haitakuwa kubwa”alisema.


Pia akiwa katika kijiji hicho,alikagua mradi wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa vinavyojengwa kupitia fedha za Maendeleo na ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya Covid-19 katika shule ya sekondari Nampungu na kutoridhishwa na kasi ya ujenzi huo.

Hivyo,amewaagiza mafundi na watendaji waliopewa dhamana ya kusimamia mradi wa ujenzi huo,kufanya kazi usiku na mchana na ukamilike haraka ili watoto waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza mwakani wayatumie madarasa hayo.

Wananchi wa kijiji hicho, wamempongeza Mbunge Kungu kutokana na jitihada mbalimbali za maendeleo anazofanya kwani katika kipindi cha mwaka mmoja tangu alipochaguliwa wilaya ya Tunduru imefanikiwa kupata miradi mingi ambayo imepunguza na kumaliza baadhi ya kero.

Hata hivyo,wananchi hao wamemuomba Mbunge Kungu, awasaidie kuwaondoa baadhi ya watumishi wa kijiji hicho ambao wanahusika kuhujumu fedha na miradi mbalimbali.

Mohamed Bwanali alisema, kuna watumishi wamekaa na kufanya kazi katika kijiji hicho kwa muda mrefu,kwa hiyo wanafanya kazi kwa mazoea jambo linalosababisha hata miradi inayopelekwa na Serikali kutosimamiwa vizuri.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.