• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MBUNGE Msongozi aiomba serikali kutekeleza miradi ya miundombinu ya barabara za Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: May 6th, 2025

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma, Mheshimiwa Jakline Msongozi, leo Mei 6, 2025, amelipamba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hotuba yake yenye msisitizo mkubwa kuhusu hali ya miundombinu ya barabara mkoani Ruvuma, akichangia bajeti ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka 2025/2026.

Akiwa amejaa shukrani na pongezi, Msongozi ameanza kwa kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri ya kuboresha miundombinu nchini, huku akimpongeza pia Waziri wa Ujenzi na Meneja wa TANROADS Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Saleh Juma, kwa usimamizi mzuri wa miradi ya barabara katika mkoa huo.

Akiweka bayana kilio chake kikuu, Mbunge huyo ameitaka serikali kutoa majibu ya kina kuhusu hatma ya barabara ya mchepuko ya Songea Mjini yenye urefu wa kilometa 16, akieleza kuwa amekuwa akiuliza swali hilo mara kadhaa bungeni bila kupata majibu yanayoridhisha. “Naibu Waziri alisema mkandarasi yuko kazini, lakini wananchi hawajashuhudia mwanzo wa ujenzi,” alisema.

Msongozi pia amegusia barabara ya kutoka Songea hadi Makambako yenye urefu wa kilometa 395, akieleza kuwa barabara hiyo imejaa mabonde na viraka, hali inayosababisha wasafiri kutumia hadi saa saba kwa safari inayopaswa kuchukua saa nne pekee. “Barabara hii ina maroli mengi ya makaa ya mawe, ni lazima ijengwe kwa haraka,” alisisitiza.

Kwa upande mwingine, Mbunge huyo ameonesha hofu juu ya kutotekelezwa kwa ujenzi wa barabara ya kimkakati ya Likuyufusi–Mkenda wilayani Songea, inayounganisha Tanzania na Msumbiji. Alisema licha ya kutengewa Shilingi bilioni 60 kwa ajili ya kilometa 60, hadi sasa hakuna hata kilometa moja iliyojengwa.

Katika wilaya ya Namtumbo, Msongozi alielezea kusikitishwa kwake na kutoanza kwa ujenzi wa barabara ya Lumecha–Londo–Mpepo yenye urefu wa kilometa 300, akiitaka serikali itangaze tarehe rasmi ya kuanza ujenzi huo ili kutoa matumaini kwa wananchi waliokuwa wakisubiri kwa muda mrefu.

Aidha, ameitaja barabara ya kimkakati ya Mtwara–Pachani hadi Tunduru yenye urefu wa kilometa 305 kuwa ni muhimu kwa maendeleo ya biashara na usafirishaji katika mikoa ya kusini, akisema hakuna taarifa za wazi kuhusu kuanza kwa ujenzi wake.

Katika hatua nyingine, Msongozi alipongeza hatua ya serikali kuanza kujenga daraja la Mkili wilayani Nyasa, akisema hatua hiyo imeleta matumaini makubwa kwa wananchi wa Nyasa, lakini akasisitiza kuwa barabara ya Mbambabay–Lituhi inayopita kandokando ya Ziwa Nyasa bado inahitaji ujenzi wa haraka kutokana na umuhimu wake wa kiulinzi na kiutalii.

Mbunge huyo aliitaka serikali kuweka kipaumbele katika ujenzi wa barabara ya Kigonsera–Mbaha kilometa 56, barabara ya Kitai–Ruanda kilometa 40 wilayani Mbinga, na kuikamilisha hadi Ndumbi wilayani Nyasa, akisema barabara hizo ni kiungo muhimu kwa uchumi na usalama wa wakazi wa Ruvuma na mikoa jirani.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.