• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MBUNGE Ruvuma akabidhi baiskeli kwa mwenye ulemavu

Imewekwa kuanzia tarehe: July 11th, 2023

MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Ruvuma Mariam Nyoka,ameifuta machozi familia ya Sophia Ali mkazi wa mtaa wa Muungano Halmashauri ya wilaya Tunduru yenye walemavu watatu baada ya kuwakabidhi jumla ya  Sh. laki 5 ili ziwasaidie kupata mahitaji yao.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo Nyoka alisema,fedha hizo ni kwa ajili ya mtaji wa kuanzisha biashara ndogo ndogo ambayo itawawezesha kupata mahitaji yao ya kila siku kutokana na kukabiliwa na hali ngumu ya maisha.

Alisema,hiyo siyo mara  ya kwanza  kutoa msaada kwa familia hiyo ambapo awali alitoa baiskeli ya magurudumu matatu kwa Sophia ili  iweze kumsaidie katika shughuli zake za kawaida.

Alisema,kama Mbunge ana wajibu wa kuwasaidia watu mbalimbali waliopo katika jamii na ni fahari kubwa kwake kuona ametimiza ahadi yake kwa familia hiyo.

“nitaendelea kuisaidia jamii ya watu wenye mahitaji muhimu kadri nitakavyoweza,hii siyo mara yangu ya kwanza kutoa msaada kwa familia ya Sophia Ali,mwezi Machi nilikabidhi baiskeli ili iweze kumsaidia mama yetu katika shughuli zake za kila siku”alisema.

Aidha,amewaomba viongozi wa Chama cha Mapinduzi kuwa na  utaratibu wa kuwaibua na kuwatambua watu wenye mahitaji maalum waliopo katika jamii ili waweze kusaidiwa.

Alisema,hatua hiyo itasaidia sana watu hao bila kujali itikadi za vyama kupata msaada kutokana na mahitaji yao na kuwaomba wadau mbalimbali kujitokeza ili kuisaidia familia hiyo yenye changamoto nyingi za maisha.

Akizungumza huku akitokwa na machozi ya furaha Sophia Ali amemshukuru Mbunge huyo kuwapatia msaada huo na kueleza kuwa,atatumia fedha hizo kwa ajili ya kuanza kujenga nyumba kuishi.

Alisema,kwa sasa anakabiliwa na hali ngumu ya maisha yeye na familia yake  kwani sehemu kubwa ya maisha yao wanategemea kupata ridhiki kupita mitaani kwa ajili ya kuomba,na kuwaomba watu wenye uwezo kuwasaidia.

Kwa upande wake katibu wa Jumuiya ya umoja wa wanawake(UWT)wilayani Tunduru Clementina Kasajo, amehaidi kuwa karibu na familia hiyo ili fedha na misaada inayotolewa na wadau kwa ajili ya familia hiyo zifanye kazi inayokusudiwa.

Mwenyekiti wa UWT wilayani humo alisema,hiyo ni mara ya kwanza tangu aingie madarakani kuona Mbunge wa viti maalum kuwajali na kuwatambua watu wenye mahitaji maalum na kuwapatia msaada.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.