• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MBUNGE wa Viti Maalum Ruvuma ashauri mitungi ya gesi ya kupikia iwekewe ruzuku

Imewekwa kuanzia tarehe: February 3rd, 2024


MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma Mheshimiwa Jacqueline Msongozi ameishauri serikali kupitia Wizara ya Nishati kuangalia uwezekano wa kuweka ruzuku kwenye mitungi ya gesi ya kupikia ili kupunguza bei ya mitungi hiyo kwa wananchi.

Akizungumza Bungeni jijini Dodoma Mbunge huyo ameshauri serikali kuongea na wadau mbalimbali ili kuondoa gharama kubwa ya ununuzi wa  mitungi ya gesi ya kupikia wakati mchakato wa kupunguza gesi hiyo  unaendelea serikalini.

Amesema gesi ya asilia inapunguza gharama kubwa kwa matumizi ya kupikia ukilinganisha na matumizi ya kuni na mkaa ambavyo vinagharama kubwa pia vinachafua mazingira.

Ameshauri serikali kuangalia namna inavyoweza kuweka mfumo wa gesi asilia kwenye Taasisi zote za serikali kikiwemo Chuo cha Ualimu Matogoro Songea na katika shule za sekondari mkoani Ruvuma na nchi nzima kwa ujumla.

Akizungumza bungeni Dodoma Naibu Waziri wa Nishati Mheshimiwa Judith Kapinga amesema agenda ya nishati safi ya kupikia ni ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan hivyo Wizara ya Nishati imelibeba suala hilo kwa uzito wa kipekee.

Kuhusu Ruzuku kwenye nishati safi ya kupikia,amesema kuna program inayowawezesha mawakala kuwezeshwa kifedha ili  kupunguza bei ya mitungi ya gesi kwa  wanaonunua gesi kwa mara ya kwanza.

“Serikali itaendelea kubuni miradi ya kupunguza bei ya mitungi ya gesi  na kutafuta fedha ili kuhakikisha wananchi wanapata mitungi ya gesi kwa gharama rahisi zaidi’’,alisisitiza Naibu Waziri wa Nishati.

Kuhusu kuwekeza mifumo ya gesi asilia kwenye Taasisi ,Mheshimiwa Kapinga amesema kupitia  Wakala wa Nishati vijijini REA umeanzishwa mradi kwa ajili ya kuweka nishati safi ya kupikia ya gesi kwenye magereza,kambi za jeshi Pamoja na shule za msingi na sekondari.

Hata hivyo amesema Wizara itaendelea kutafuta fedha ili kuhakikisha mifumo ya nishati safi ya kupikia inazifikia Taasisi nyingi zaidi zikiwemo Taasisi za elimu mkoani Ruvuma.

Sera ya Taifa ya mwaka 2015 inaielekeza serikali kuchukua hatua Madhubuti ili kufanikisha matumizi ya nishati safi,

 Hivi sasa serikali inakamilisha kuandaa mkakati wa Taifa wa  matumizi safi ya nishati  ya kupikia kwa lengo la kuhakikisha asilimia 80 ya watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2033.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini GCU Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvum

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • KIONGOZI Mwenge wa uhuru ashiriki upandaji miti Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru waweka jiwe la msingi shule ya amali Songea

    May 11, 2025
  • MWENGE wa uhuru wazindua jengo la EMD Peramiho

    May 10, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.