• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MFUMO wa stakabadhi ghalani ulivyowaingizia mabilioni wakulima wa Songea na Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: September 1st, 2021

MFUMO wa stakabadhi ghalani umewaingizia wakulima wa Wilaya za Songea na Namtumbo mkoani Ruvuma mabilioni ya fedha tangu ulipoanza kutumika mwaka 2019.

Akizungumza wakati anatoa taarifa ya uendeshaji wa Chama Kikuu cha Ushirika SONAMCU Ltd kwa Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Ruvuma,Meneja Mkuu wa Chama hicho Juma Mwanga amesema wakulima wamepata mafanikio makubwa katika mazao ya ufuta,soya na mbaazi yaliouzwa kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani.

Mwanga amesema katika kipindi cha mwaka 2019 hadi 2021,kupitia zao la ufuta,wakulima waliuza kilo 19,163,454 na kufanikiwa kupata zaidi ya shilingi bilioni 45,huku Halmashauri zikipata mapato ya zaidi ya bilioni 1.9,SONAMCU ilipata zaidi ya milioni 574 na vyama vya msingi zaidi ya shilingi bilioni1.341.

Amesema katika kipindi hicho cha miaka mitatu katika zao la soya ziliuzwa jumla ya kilo 5,550,290 na wakulima kuingiza zaidi ya shilingi bilioni 4.925,mapato ya Halmashauri zaidi ya shilingi milioni 156,SONAMCU zaidi ya milioni 84 na mapato ya vyama vya msingi ni zaidi ya milioni 194.

Kulingana na Meneja Mkuu huyo wa SONAMCU,katika kipindi cha mwaka 2019 hadi 2021 katika zao la mbaazi kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani ziliuzwa kilo 4,920,996 ambazo ziliwaingizia wakulima zaidi ya shilingi bilioni nne,Halmashauri ilipata zaidi ya shilingi milioni 143,SONAMCU ilipata  zaidi ya milioni 59 na vyama vya msingi vilipata zaidi ya shilingi milioni 129.

“Mfumo wa stakabadhi ghalani una faida nyingi zikiwemo wakulima kukutanishwa na wanunuzi hivyo kuwafanya wawe na maamuzi ya kuuza mazao yao kwa umoja wao na kuwepo kwa matumizi ya vipimo halali vya wakulima kwa sababu wanunuzi hutumia mizani iliyohakikiwa na wakala wa vipimo’’,alisisitiza Mwanga.

Amezitaja faida nyingine za mfumo huo kuwa ni upatikanaji wa tozo za serikali kwa njia rahisi,kuongezeka kwa bei ya mazao ya ufuta,soya na mbaazi ambao umetokana na kuongezeka kwa wanunuzi ambao wanashindanishwa kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani na kutoa bei kubwa kwa wakulima.

Faida nyingine za mfumo huo ni kufufuka kwa vyama vya ushirika toka 24 vilivyokuwa vinauza tumbaku tu hadi kufikia 63 ambavyo vinauza mazao ya ufuta,soya na mbaazi.

Chama kikuu cha SONAMCU ambacho kiliandikishwa mwaka 2013 hivi sasa kina wanachama 46 wa vyama vya msingi.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ametoa rai kwa vyama vya ushirika kuendelea kutoa elimu ya faida kwa mfumo huo kwa wanachama wao ili wakulima wengi wautumie na kupata bei yenye tija.

Ametoa rai kuangalia wakulima wengi zaidi kujiunga na mfumo huo ili kupata tija katika mazao yao hivyo  ameagiza vyama vya kushirika kuongeza uaminifu kwa watendaji na kuzingatia maslahi ya wanachama ambapo ametaka kuachana na maslahi binafsi ambayo yanarudisha nyuma ushirika.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Septemba Mosi,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.