• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MFUMO wa stakabadhi ghalani waleta manufaa kwa wakulima wa Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: August 25th, 2021

BEI ya kuuza mbaazi za wakulima katika wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani imezidi kupanda zaidi kutoka wastani wa Sh.1,294  hadi kufikia Sh.1,341 kwa kilo moja.

Afisa Ushirika wa wilaya ya Tunduru George Bisani amesema,katika minada yote miwili jumla ya kilo 1,505,849  kati ya hizo kilo 360,551 zimeuzwa katika mnada wa kwanza kwa bei ya  Sh.1,294 kwa kilo moja.

Amesema, katika mnada wa pili uliofanyika katika kijiji cha Semeni jumla ya kilo 1,145,498 zimeuzwa kwa bei ya Sh.1,391 na kufanya jumla ya fedha zote zilizoingia kwenye mzunguko kutokana na minada  miwili ya mbaazi wilayani Tunduru kufikia Sh. Bilioni 1,536,167,320.00.

Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Chama Kikuu cha Ushirika wilaya ya Tunduru(Tamcu Ltd)Imani Kalembo amesema, huo ni mnada wa pili  wa zao la mbaazi kufanyika katika wilaya hiyo katika msimu wa kilimo wa mwaka 2020/2021.

Kalembo amesema, katika mnada huo makampuni matano yamejitokeza kununua mbaazi na kampuni ya Lenic Tanzania Ltd imeshinda  kutokana na kutangaza  bei ya Sh.1,341 kwa kilo moja ikiyazidi makampuni mengine.Amesema, katika mnada huo jumla ya tani 1,042 sawa na kilo 1,145,498 zimeuzwa ambapo bei ya kilo moja  ya mbaazi ni Sh.  1,341.

Amesema, Chama Kikuu cha Ushirika kina furaha kuona bei ya mbaazi  inaongezeka katika kila  mnada  kutoka Sh.1,294 katika mnada wa kwanza uliofanyika  katika kijiji cha Mtonya hadi  kufikia Sh 1,341 mnada wa pili uliofanyika kijiji cha Semeni.

Amewataka wakulima kutokubali kushawishika na wanunuzi wa kati wanaonunua mbaazi kwa bei ndogo ya Sh. 800 kwa kilo ambayo haina faida, badala yake kuendelea kuuza mbaazi zao  mfumo wa stakabadhi ghalani kupitia vyama vya msingi vya ushirika.

Ametoa wito kwa makampuni  mbalimbali,kwenda katika wilaya hiyo kununua mbaazi ambazo zinapatikana kwa wingi na kuhakikisha wananunua kwa bei nzuri ili kuhamasisha wakulima waweze kuzalisha kwa wingi.

Baadhi ya wakulima wa mbaazi katika kijiji hicho wameishukuru  Serikali kwa kuliingiza zao  hilo katika mfumo wa stakabadhi ghalani kwa kuwa umewasaidia  kupata soko la uhakika na bei nzuri kutoka Sh. 250  hadi 300 kwa kilo moja.

Wamesema, kuanzishwa kwa  mfumo wa stakabadhi ghalani kwa zao la mbaazi na mazao mengine ya kimkakati ikiwemo zao maarufu la korosho kumewasaidia  kuwa na uhakika wa bei nzuri na kuepuka kulanguliwa na wanunuzi wa mitaani wasiokuwa  na huruma kwao.

Hadija Omari(43)amesema, kama serikali itaendelea na kusimamia mpango wa kuuza mbaazi kwa mfumo wa stakabadhi ghalani basi wakulima wengi watahamasika kuongeza uzalishaji na hivyo kuondokana na umaskini katika familia zao.

Ameitaka Serikali kuhakikisha inawabana na kuwachukulia hatua kali baadhi ya wanunuzi wachache wanaopita mashambani na vijijini kuwalaghai wakulima, ili wauze mbaazi kwa bei ndogo isiyolingana na gharama halisi za uzalishaji.

Omari Misoya amesema, licha ya malipo kuchelewa  mara wanapouza,lakini mfumo wa stakabadhi ghalani umesaidia kupata bei nzuri ya mbaazi wanazolima ikilinganisha na bei za walanguzi wa mitaani.

Amesema,mfumo  huo umeleta heshima kubwa  kwa mkulima na pia usalama wa fedha wanazolipwa kwani zinapitia moja kwa moja benki badala ya kupewa mkononi jambo ambalo ni hatari kwa maisha yao.Hata hivyo, ameiomba Serikali kuyabana makampuni yanayonunua  mbaazi kulipa fedha  kwa wakulima haraka ili waweze kutatua changamoto zinazowakabili kwenye familia zao  mahitaji ya shule kwa Watoto wao.

Imeandikwa na Muhidin Amri Tunduru


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.