• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MFUMO wa stakabadhi za ghala wawaingizia wakulima Tunduru bilioni 33

Imewekwa kuanzia tarehe: May 15th, 2023

WAKULIMA wa mazao ya ufuta,mbaazi na korosho wanaohudumiwa na Chama Kikuu cha Ushirika wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma(TAMCU),katika msimu wa kilimo wa mwaka 2022/2023 wamelipwa zaidi ya Sh.bilioni 33 kupitia vyama vya msingi vya ushirika(Amcos).

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa TAMCU Mussa Manjaule wakati akitoa taarifa ya chama hicho kwenye mkutano mkuu wa Tamcu uliofanyika katika ukumbi wa Sky Way mjini Tunduru.

Manjaule alisema,Chama kikuu cha Ushirika(Tamcu Ltd)kinachosimamia mauzo ya zao la korosho katika mikoa ya Njombe,Ruvuma na Mbeya katika msimu wa kilimo 2022/2023 kilifanikiwa kukusanya  jumla ya kilo 20,802,513 ya mazao matatu ya Ufuta,mbaazi na korosho ambapo kati ya hizo korosho zilikuwa kilo 15,218,006 zenye thamani ya Sh.bilioni 26,917,916,197.03 na wakulima walilipwa Sh.bilioni 23,312,161,64.

Alisema,kwa upande wa zao la ufuta walikusanya kilo 2,548,815 zenye thamani ya Sh.bilioni 7,710,907,700.00 ambazo ziliwaingizia wakulima  Sh.bilioni 7,498,081,647.5 na mbaazi  zilipatikana kilo 3,035,692 zenye thamani ya Sh.bilioni 2,633,233,689.53  na wakulima walilipwa Sh.bilioni 2,475,377,705.5.

Aidha alisema,katika msimu wa kilimo 2022/2023 licha ya kuwa na hali mbaya ya hewa iliyoambatana na mvua zisizoeleweka ambayo kwa kiasi kikubwa ilichangia kupunguza ubora wa mazao hasa korosho wakati wa uvunaji,lakini wamefanikiwa kudhibiti ubora wa mazao.

Kwa mujibu wa Manjaule,hali hiyo imetokana na usimamizi na operesheni za mara kwa mara zilizofanywa na kamati ya ulinzi na usalama ikiongozwa na Mkuu wa wilaya Julius Mtatiro kwa kushirikiana na  wajumbe wa bodi ya Tamcu Ltd na vyama vya Ushirika vya msingi.

Alisema kuwa,ushuhuda wa ubora wa mazao hayo uliwavutia hata wanunuzi ambao walikiri kuwa ni safi ambapo kwa upande wa korosho kati ya kilo 15,218,006 zilizouzwa mnadani kilo 14,845,624 zilikuwa daraja la kwanza na kilo 372,382 daraja la pili.

Kwa upande wake meneja wa Chama Kikuu cha Ushirika wilayani humo(Tamcu Ltd)Iman Kalembo alisema,katika msimu 2022/2023 Tamcu imeendesha jumla ya minada 11 ya mauzo ya korosho ghafi na kuuza kilo 15,281,006 zenye thamani ya Sh.bilioni 26,291,272,829.

Alifafanua kuwa,kati ya kilo hizo mkoa wa Ruvuma ulizalisha kilo 15,156,209 sawa na asilimia 99.5,mkoa wa Njombe ulizalisha kilo 35,947 sawa na asilimia 0.24 na kilo25,850  sawa na asilimia 0.17 zilitoka mkoa wa Mbeya.

Alisema,uzalishaji wa korosho umeshuka kutoka kilo 25,284,493 kwa msimu 2021/2022 hadi kilo 15,218,006 kwa msimu 2022/2023 ambapo ni sawa na anguko la asilimia 39.81.

Kalembo alisema,changamoto ya kushuka kwa uzalishaji na ubora wa korosho,ilichangia hata kushuka kwa bei katika soko la Dunia ambapo korosho daraja la kwanza iliuzwa kwa bei ya juu Sh. 1,905 na ya chini Sh.1,600 na kufanya  wastani wa bei kwa korosho za daraja la kwanza Sh. 1,742 na daraja la pili bei ya juu Sh.1,370 na bei ya chini Sh.1,340.

Aliongeza kuwa, wastani wa bei ya korosho kwa msimu 2022/2023 ni Sh.1,357 ikilinganishwa na msimu 2021/2022 ambapo korosho zote ziliuzwa daraja la kwanza na bei ya juu ilikuwa Sh.2,157 na bei ya chini Sh.1,700.

Mkuu wa wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro,amewapongeza wakulima kwa kuendelea na uzalishaji wa zao hilo na viongozi wa vyama vya msingi na Chama Kikuu cha Ushirika(Tamcu Ltd)kwa usimamizi mzuri na kumaliza madeni ya fedha za wanachama wao.

Alisema,hali hiyo imetokana na viongozi waliopo kufuata kanuni,sheria na taratibu za Ushirika ambazo zimesaidia kuimarisha sana Amcos na wakulima kulipwa stahiki zao,tofauti na miaka ya nyuma ambapo kulikuwa na ubabaishaji mkubwa kila inapofika wakati wa msimu wa mauzo ya korosho.

Amewataka viongozi wanaosimamia vyama vya ushirika,kuwa waadilifu,waaminifu,kutenda haki na kutekeleza majukumu yao kwa wakati, badala ya kuvitumia vyama hivyo kama  taasisi ya familia au sehemu ya kutafuta nafasi za uongozi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.