• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MIAKA minne ya Rais Dkt.Samia ilivyoboresha sekta ya afya Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: April 16th, 2025

Na Albano Midelo

Katika miaka minne iliyopita, sekta ya afya nchini Tanzania, hasa katika mkoa wa Ruvuma, imepiga hatua kubwa kwa juhudi za serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dr.Louis Chomboko anasema Kupitia uwekezaji wa miundombinu, rasilimali watu, na huduma za afya za msingi, maendeleo yamekuwa dhahiri huku wananchi wakishuhudia maboresho makubwa katika upatikanaji wa huduma bora za afya.

Ongezeko la Vituo vya Afya na Rasilimali Watu

Mkoa wa Ruvuma una jumla ya vituo 473 vya huduma za afya, ikiwa ni pamoja na hospitali 18, vituo vya afya 50, na zahanati 341.

Hata hivyo Serikali inamiliki sehemu kubwa ya vituo hivi, ikiwa na hospitali tisa, vituo vya afya 39, na zahanati 277. Pamoja na ongezeko hili, upatikanaji wa watumishi wa afya uko katika asilimia 47.2 huku mahitaji yakiwa watumishi 7,043 dhidi ya waliopo 3,323.

Maboresho ya Huduma za Afya Kupitia Teknolojia

Katika kuhakikisha huduma za afya zinaboreshwa, mfumo wa kielektroniki wa serikali (GoTHOMIS) umesimikwa katika vituo 192 kati ya 325, sawa na asilimia 64.74, huku lengo likiwa ni kufikia vituo vyote.

Upatikanaji wa Dawa na Vifaa Tiba

Upatikanaji wa dawa na vifaa tiba umeongezeka kutoka asilimia 50 mwaka 2021 hadi asilimia 84 mwaka 2024. Hii ni kutokana na usimamizi thabiti wa serikali, pamoja na ongezeko la ruzuku kwa vituo vya afya.

 Kiasi cha  shilingi bilioni 7.95  kilitolewa kwa ajili ya dawa na vifaa tiba, huku asilimia 90.1 ya bidhaa zilizohitajika zikifikishwa kwenye vituo vya afya.

Mafanikio Katika Huduma za Chanjo

Katika kipindi cha miaka minne, huduma za chanjo zimeimarika, huku baadhi ya chanjo zikifikia viwango vya juu zaidi ya asilimia 100 ya malengo yaliyowekwa. Mfano, chanjo ya kifua kikuu (BCG) imefikia asilimia 166, polio asilimia 135, na HPV asilimia 126.

Huduma za Uzazi na Mtoto

Mkoa wa Ruvuma una vituo 348 vinavyotoa huduma za afya ya uzazi na mtoto, ambapo vituo 325 vinatoa huduma ya chanjo na vituo 313 vinatoa huduma ya uzazi na kujifungua.

Huduma za Saratani ya Mlango wa Kizazi

Jumla ya wanawake 22,718 walichunguzwa saratani ya mlango wa kizazi, ambapo 301 (asilimia 1.3) waligundulika kuwa na VIA positive na asilimia 87 walitibiwa. Wanawake 79 walihisiwa kuwa na saratani na kupatiwa rufaa kwa uchunguzi zaidi.

Huduma za Ustawi wa Jamii na Mfuko wa Afya (iCHF)

Mpango wa usajili wa watoto chini ya miaka mitano umefanikiwa kwa asilimia 119.9, huku watoto 283,094 wakiwa wameandikishwa. Aidha, kaya 31,767 zimejiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa (iCHF), zikichangia shilingi milioni 953 .

Uwekezaji katika Huduma za Maabara na Uchunguzi wa Magonjwa

Mkoa umepokea mashine za kisasa za uchunguzi wa magonjwa, ikiwa ni pamoja na mashine 27 za hematolojia, 26 za biochemistry, mashine tisa za Genexpert kwa uchunguzi wa kifua kikuu na  mashine nane za X-ray za kidijitali ambazo zimepelekwa kwenye hospitali mbalimbali.

Maendeleo ya Miundombinu ya Afya

Serikali imewekeza zaidi ya shilingi bilioni 4.76  katika miradi 29 ya afya, ambapo miradi 2 imekamilika kwa asilimia 100 na mingine 27 ipo katika hatua mbalimbali za umaliziaji. Kwa mwaka 2024/2025, Tsh 3.42 bilioni zimetengwa kwa miradi mipya.

Mafanikio haya yanaonesha dhamira ya serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha sekta ya afya, kwa maendeleo endelevu ya sekta ya afya nchini Tanzania.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • BODI ya kwanza ya maji yazinduliwa Tunduru

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.