• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MIAKA minne ya Rais Samia ilivyoongeza uzalishaji wa madini Ruvuma na mapato ya serikali

Imewekwa kuanzia tarehe: March 1st, 2025

Picha juu ni Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan wakati anazindua soko jipya la madini ya dhahabu na  vito wilayani Tunduru

Uzalishaji wa madini ya makaa ya mawe katika Mkoa wa Ruvuma umeendelea kuwa chanzo muhimu cha mapato ya serikali katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa serikali ya  Awamu ya Sita ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Katika mwaka wa fedha 2023/2024, serikali iliuza tani 1,356,249.84 za makaa ya mawe zenye thamani ya zaidi ya Dola milioni 144.9 za Marekani.

 Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Alphonce Bikulamchi, amesema kupitia mauzo hayo, serikali ilikusanya mrabaha wa Dola 3,937,434.98 na ada ya ukaguzi ya Dola 914,034.68. Madini hayo yameuzwa ndani ya nchi na kusafirishwa katika nchi jirani, barani Ulaya na Asia kupitia bandari za Mtwara na Dar es Salaam.

“Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Ruvuma imeendelea kutoa leseni za uchimbaji na biashara ya madini, ikiwemo leseni za uchimbaji mdogo (PML) na leseni za madini ya biashara kwa madalali (Dealers na Brokers), idadi ya leseni zilizotolewa imekuwa ikiongezeka, ambapo kwa mwaka wa fedha 2021/2022 hadi 2024/2025, mkoa una jumla ya leseni 144 za utafutaji madini na uchimbaji mkubwa na wa kati’’,alisema Mhandisi Bikulamchi,

 Kwa mujibu wa Bikulamchi,Katika ukusanyaji wa maduhuli, Ofisi ya Madini Mkoa wa Ruvuma ilikusanya jumla ya shilingi 105,120,541,415.03 kati ya mwaka wa fedha 2021/2022 hadi 2024/2025, sawa na asilimia 126 ya lengo la makusanyo.

 Mhandisi Bikulamchi anasema ongezeko la makusanyo haya ni ishara ya usimamizi mzuri wa sekta ya madini na kuimarika kwa mauzo ya madini hayo.

Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa michache nchini iliyobarikiwa kuwa na utajiri wa madini ya aina mbalimbali

Picha chini ni Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa alipotembelea Mgodi wa makaa ya mawe wa JITEGEMEE wilayani Mbinga


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.