• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MIFUMO ya utoaji haki nchini iboreshwe kuleta haki na usawa kwa jamii

Imewekwa kuanzia tarehe: February 1st, 2024

JAJI Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Songea Mheshimiwa James Karayemaha amesema mifumo ya utoaji na upatinaji haki nchini ni muhimu kuboreshwa na kuimarishwa ili iweze kuleta usawa na ustawi katika jamii.

Jaji Karayemaha amesema hayo  wakati anazungumza kwenye  kilele cha maadhimisho ya siku ya sheria nchini ambazo kimkoa zimefanyika kwenye viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Songea.

Amebainisha kuwa utoaji na upatikanaji wa haki utawezekana ikiwa kutakuwa na mifumo imara na jumuishi baina ya Taasisi hususan kwenye eneo la vitendea kazi vya kisasa vya TEHAMA na uwepo wa miundombinu wezeshi baina ya Taasisi ya haki jinai.

“Mahakama imekuwa ikifanya maboresho kwenye huduma zake ili kutoa huduma bora inayomlenga mwananchi kupitia Mpango Mkakati wa miaka mitano ambao umesimikwa katika nguzo tatu zinazoongoza  katika utekelezaji  na Programu za kimaboresho’’,alisisitiza Jaji Mfawidhi.

Amezitaja nguzo hizo kuwa ni mahakama kutekeleza utawala bora,uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali,upatikanaji na utoaji wa haki kwa wakati na  kuthamini imani kutoka kwa wananchi,watumiaji wa huduma za mahakama na jamii kwa ujumla.

Akizungumzia umuhimu wa mfumo jumuishi Jaji Mfawidhi huyo Mahakama Kuu Kanda ya Songea,amesisitiza kuwa kuanzishwa kwa Mfumo Jumuishi wa Taasisi za Haki Jinai utasaidia upatikanaji wa taarifa kwa wakati muafaka,kuondoa urasimu na utendaji kazi katika hatua mbalimbali zilizopo kwenye Taasisi za Haki Jinai hivyo haki kutolewa kwa wakati.

Hata hivyo  amesema TEHAMA ina nafasi kubwa  katika kuboresha haki na kufanikisha upatikanaji wa haki kwa wakati ambapo amesema Mahakama inaendelea kuboresha huduma zake kupitia mifumo ya TEHAMA.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas akizungumza kwenye kilele cha maadhimisho hayo ameipongeza Idara ya Mahakama Kuu Kanda ya Songea kwa kupiga hatua kubwa katika utoaji haki hasa baada ya kuboresha miundombonu ya mahakama ikiwa ni Pamoja na matumizi ya TEHAMA.

RC Thomas ameipongeza Mahakama Kuu Kanda ya Songea kwa kutatua changamoto ya mlundikano wa mashauri ambapo hivi sasa mashauri yenye muda mrefu yamebakia machache.

Ameipongeza Mahakama hiyo kwa kupeleka  vifaa vya TEHAMA katika magereza  ya Tunduru na Mbinga ambavyo vinakwenda kutumika kwa ajili mfumo wa jumuishi wa haki jinai kwa ajili ya kusikiliza mashauri kwa njia ya mtandao.

Amesisitiza kuwa juhudi zinazofanywa na vyombo vyote vya haki jinai zina mchango mkubwa kwa jamii ambapo ameshauri kushirikiana ili kuunganisha mifumo ya utendaji kazi hatimaye kufikia mafanikio makubwa katika utoaji haki.

Kaulimbiu ya mwaka huu kwenye maadhimisho ya siku ya sheria nchini inasema umuhimu wa dhana ya haki kwa ustawi wa Taifa;nafasi ya mahakama na wadau katika kuboresha mfumo jumuishi na haki jinai.Baadhi ya Mahakimu  kutoka Kanda ya Songea wakiwa kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya sheria nchini  

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.