• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MILIONI 110 zakamilisha mradi wa bweni la sekondari ya Chabruma Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: May 15th, 2023

SERIKALI imetumia kiasi cha Sh.milioni 110 kukamilisha ujenzi wa Bweni la wanafunzi wa kike katika shule ya sekondari Chabruma kata ya Lilambo katika manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa bweni hilo kwa Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Kanal Laban Thomas,Mkuu wa shule hiyo Sikudhan Komba alisema ujenzi wa bweni hilo umetekelezwa kwa awamu tatu.

Komba alisema,katika awamu ya kwanza  kwa mwaka wa fedha 2020/2021 walipokea Sh.milioni 80

ikiwa ni fedha za mradi EP4R.Alisema,katika awamu ya pili mwaka 2021/2022 walipokea Sh.milioni 8 kutoka mfuko wa Jimbo na awamu ya tatu 2022/2023 wamepokea Sh.milioni 22 fedha kutoka serikali kuu.

Alisema,kukamilika kwa mradi huo kumewasaidia watoto wa kike 74 kuishi bwenini na hivyo kupunguza adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kutoka maeneo wanayoishi.

Aidha alisema,wanafunzi wanapata muda wa ziada wa kujisomea,kuepukana vishawishi mbalimbali,kuongeza ufaulu na utawasaidia wanafunzi wa kike kuweza kutimiza ndoto zao.

Akizungumza baada ya kuzindua bweni hilo Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Kanal Laban Thomas,amewataka wanafunzi kusoma kwa bidii ili waweze kutimiza ndoto zao na kuepuka kupokea zawadi kwa watu wenye nia ovu hasa kwa watoto wa kike.

Alisema,serikali ya awamu ya sita imejitahidi sana kujenga na kuboresha miundombinu ya elimu inayomsaidia mwanafunzi kusoma katika mazingira  mazuri na walimu kuwa na sehemu nzuri ya kufundishia.

Kanal Laban,amewaasa wanafunzi kuzingatia masomo na kuzingatia maadili ya kitanzania  na kuepuka kujiingiza kufanya vitendo vinavyokwenda kinyume na maadili ambavyo kwa sehemu kubwa vina wadhalilisha hasa vijana wa kiume kutokana na tamaa ya kupata mali.

Amewataka wanafunzi kutunza bweni hilo na miundombinu mingine ya shule,ili iweze kudumu kwa muda mrefu na iwasaidie katika kutimiza ndoto zao badala ya kuwa sehemu ya waharibifu wa miundombinu hiyo inayojengwa kwa fedha nyingi za serikali.

Katika hatua nyingine Mkuu wa mkoa,amewakumbusha Watanzania kuhusu umuhimu wa kudumumisha muungano na amani ya nchi yetu kwa kutokubali kushawishiwa kwa namna yoyote kujaribu kuvunja muungano wetu ambao ni mawazo mazuri ya waasisi wa Taifa letu Hayati Mwalimu Julius Nyerere na  Abeid Aman Karume.

“wanangu mjitahidi kusoma kwa bidii kwani elimu ndiyo itawakomboa katika maisha yenu,elimu ndiyo itatufanya tuendelea kudumisha na kusimamia muungano wetu kwa kujua faida na manufaa yake,tusiposoma itakuwa rahisi kudanywa kuhusu muungano wetu”alisema Kanal Laban.

Alisema,muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni wa aina yake Duniani na haupatikani sehemu yoyote na unatoa fursa kwa kila Mtanzania kuwa na haki ya kuwekeza kitu chochote ndani ya Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.