• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MILIONI 400 zilivyojenga hosteli katika sekondari tano Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: March 7th, 2021

HALMASHAURI ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma imetumia kiasi cha shilingi milioni 400 kujenga hosteli tano katika shule za sekondari ili kuwapunguzia kero wanafunzi wa kike.

Afisa Mipango wa Halimashauri hiyo Athumani Nyange amesema  kila hosteli imegharimu shilingi milioni 80 na kwamba fedha zilizotumka kutekeleza mradi huo zimetolewa na serikali kwa ajili ya kujenga hosteli katika shule za sekondari Matimira, Kilagano,Maposeni,Mpitimbi na Mhalule

Nyange amesema Halmashauri ilipokea fedha hizo Agosti 2020 kwa ajili ya kutekeleza mradi huo ambapo ujenzi umekamilika kwa asilimia 100 na kwamba hivi sasa kinachosubiriwa ni kuweka vitanda na hosteli kuanza kutumika rasmi.

“Kila hosteli  ina uwezo wa kubeba wanafunzi 80,kila hosteli ina vyumba 20,kila chumba kinachukua wanafunzi wanne kwa niaba ya wananchi tunaishukuru sana serikali kwa sababu hosteli hizi ni ukombozi kwa watoto wa kike’’,alisema Nyange.

Selestin Mlelwa ni Kaimu Mkuu wa shule ya sekondari  Mhalule  amesema mradi wa hosteli katika shule hiyo umekamilika na kusisitiza kuwa hosteli hiyo itakuwa ukombozi kwa watoto wa kike ambao wamekuwa wanatembea kilometa tisa kila siku kwenda na kurudi shuleni.

Patrick Matembo ni Mkuu wa shule ya sekondari Mpitimbi  anaishukuru serikali kwa kuipatia shule hiyo zaidi ya shilingi milioni 106 kwa  ajili ya kutekeleza miradi mitatu ambayo ni hosteli moja imegharimu sh. milioni 80,darasa moja sh. milioni 20 na ujenzi wa choo matundu sita uliogharimu sh.milioni sita.

Elizabeth Mwakyusa ni mwanafunzi wa kidato cha sita sekondari ya Mpitimbi anatoa shukrani kwa serikali kwa kuwajengea hosteli kitendo ambacho amesema kitawaongezea wanafunzi ari ya kusoma na kuongeza ufaulu sanjari na kupunguza utoro ambao ulikuwa unachangiwa na kutembea kwa umbali  mrefu kutoka kwenye makazi yao.

Halmashauri ya wilaya ya songea ina jumla ya shule za sekondari   21 kati ya hizo sekondari 16 zinamilikiwa na serikali na  sekondari tano zinamilikiwa watu binafsi na Taasisi ya dini.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Machi 7,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.