• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MILIONI 560 zilivyojenga sekondari mpya ya mfano Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: May 11th, 2023

SERIKALI imetoa shilingi milioni 560.6 kutekeleza mradi wa ujenzi wa sekondari mpya ya Kungu katika Kata ya Nakayaya wilayani Tunduru mkoani Ruvuma.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa sekondari hiyo kwa sekretarieti ya Mkoa ikiongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Ndugu Stepehen Ndaki,Mkuu wa shule ya sekondari Kungu Ayubu Kundya amesema ujenzi huo umetekelezwa kupitia program ya uboreshaji elimu ya Sekondari (SEQUIP).

Kundya amezitaja shughuli ambazo zimekamilika katika utekelezaji wa mradi huo kuwa ni ujenzi wa madarasa manane,ujenzi wa jengo la utawala, maabara,jengo la TEHAMA,maktaba,uchimbaji wa kisima na uchongaji wa barabara.

“Shule imekamilika na imechukua wanafunzi ndani ya kata za Nakayaya na Masonya ambapo kwa mwaka 2023 jumla ya wanafunzi 220 walipangiwa kuanza kidato cha kwanza katika shule hiii’’,alisema.

Hata hivyo amesema hadi kufikia Machi 31 mwaka huu wanafunzi walioripoti katika shule hiyo ni 205 ambapo amezitaja changamoto zinazosababisha mradi huo kushindwa kutekelezwa kwa asilimia 100 kuwa ni  mabadiliko ya bei za viwandani,ukosefu wa bomba la kupandishia maji kwenye tanki na ukosefu wa umeme.

Akizungumza mara baada ya kukagua mradi huo,Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Ndugu Stephen Ndaki ameipongeza Halmashauri ya Tunduru kwa kusimamia ipasavyo mradi huo ambao umeanza kutumika.

Hata hivyo Ndaki ameagiza changamoto zilizopo zipatiwe ufumbuzi ili mradi uweze kutoa huduma kwa asilimia 100 hivyo kuwa na mazingira rafiki ya kujifunzia.

Serikali kupitia program ya SEQUIP imejenga sekondari mpya tatu katika wilaya ya Tunduru ambapo kila shule imepewa shilingi milioni 470.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.