• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MILIONI 62 kuimarisha zao la ufuta na soya Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: April 6th, 2024


HALMASHAURI ya wilaya Namtumbo mkoani Ruvuma,imetenga Sh.milioni 62,500,000 kwa ajili ya kuboresha kilimo cha zao la ufuta na soya katika msimu wa kilimo 2024/2025.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Philimon Magessa amesema,fedha hizo zitatumika kuwajengea uwezo maafisa ugani na wakulima kama mpango wa Halmashauri wa kuimarisha na kuongeza vyanzo vyake vya mapato.


Amesema,kupitia mpango huo Hamashauri imehamasisha wananchi umuhimu wa kilimo cha zao la ufuta kwa kugawa mbegu bora kwa wakulima ili kuwavutia kulima zaidi zao hilo ambalo limeonesha mafanikio makubwa.

Kwa mujibu wa Magessa,hatua hiyo itasaidia wilaya ya Namtumbo kuongeza uzalishaji wa mazao ya biashara na Halmashauri kupata mapato na kukidhi mahitaji muhimu ya uendeshaji wa Halmashauri.


Amesema,kwa kuzingatia ukubwa wa eneo na uwezo wa ardhi kuzalisha mazao ya biashara Halmashauri imejipanga kuwekeza kwenye kilimo(block Farmina)kwa mazao ya Soya na Ufuta.


Ameutaja,mkakati uliopo ni kupima maeneo na kuyagawa kwa wawekezaji wazawa na wageni kwa matarajio ya kukusanya ushuru wa mazao na maeneo hayo ni Limamu ekari lenye 17,000,Ligera,Mchomoro na Likuyu.


Amesema,wameweka mikakati ya kuongeza mapato yake ya ndani ikiwemo kuhuisha na kuvijengea uwezo vyanzo vya mapato vilivyopo ili viweze kufanya vizuri zaidi.


Ameitaja mikakati hiyo ni pamoja kufanya ukarabati wmajengo yote yanayokodishwa,kuwajengea uwezo wakusanyaji wa mapato ili waweze kukusanya zaidi na kuajiri vibarua kwa ajili ya kukusanya mapato kwenye maeneo mbalimbali.


Amesema,watawajengea uwezo watendaji wa vijiji na kata juu ya mbinu sahihi za kusimamia ukusanyaji wa mapato,kutunga na kusimamia sheria ndogo za ukusanyaji wa mapato ya ndani ambayo yatachangia asilimia 0.8 ya mapato ya sasa ya Halmashauri.


Magessa amesema,mkakati huo ulianza tangu mwaka 2027/2018 unatarajia kuiwezesha Halmashauri kukusanya na kufikia malengo kwa asilimia mia moja au zaidi ifikapo mwaka wa fedha 2029/2030.


Ameongeza kuwa,wataimarisha na kusimamia sekta ya uwekezaji hasa kwenye madini yanayopatikana na katika wilaya hiyo yakiwemo madini ya Uranium,Kwatz,Makaa ya mawe,Tantalaiti,Titaniam,Manganizi na Dhahabu.


Ameyataja madini mengine kuwa ni Nobiamu, Ulanga, Lithiamu,Beriliamu,Amazonaiti,Topazi ambapo kampuni ya Mantra inafanya utafiti wa madini ya Urani katika kijiji cha Amani,kata ya Magazini na kutoka chanzo hicho Halmashauri inatarajia kupata wastani wa Sh.milioni 500.


Amekitaja,chanzo kingine ni kuuza hewa Ukaa kwa Kampuni ya Carbon Tanzania yenye makao makuu mjini Arusha ambayo imesaini mkataba na Halmashauri kwa kushirikiana na Jumuiya za hifadhi maliasili kwa jamii.


Amezitaja jumuiya hizo kuwa ni Kipalang’andu,Kimbanda na Kisungule ambapo Halmashauri itapata asilimia nane ya fedha zitakazotokana na mauzo ya kaboni na mapato yanayotarajiwa ni Sh.milioni 400.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.