• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MILIONI 699 kufungua barabara ya Muhukuru-Kizuka

Imewekwa kuanzia tarehe: July 15th, 2023

SERIKALI yatoa millioni 699 kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Mto Njoka lenye ukubwa wa mita 20 na ambalo litapitika muda wote na kusaidia kufungua barabara Muhukuru mpaka Kizuka itakayochochea uchumi kwa wananchi.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) Peramiho wakati wa ziara ya kutembelea miradi ya maendeleo katka Halmashauri ya wilaya ya Songea 

“Barabara hii ni barabara muhimu, ni barabara ya huduma ni barabara ya uchumi ni barabara itakayoimarisha ulinzi,” na kipekee ninamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja alisema Waziri Mhagama.

Waziri Mhagama alifafanua, serikali imetenga fedha kwa ajili ya kujenga daraja la mto Mgugusi kwa mwaka wa fedha 2023/2024 ili madaraja yote makubwa yaweze kupitika katika majira yote ya mwaka wakati wa mvua na wakati wa kiangazi.

Aidha ujenzi wa madaraja madogo madogo manne umekamilika na wakala wa barabara vijijini TARURA wanamalizia ujenzi wa madaraja mengine manne madogo madogo yaliyobakia katika ujenzi wa barabara.

“Ukamilishwaji wa ujenzi wa barabara utarahisishia wananchi kupata huduma ya usafiri kwa haraka na kuchochea ukuaji wa Miji,” alisema

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Songea Mhe. Menas Komba amesema ujenzi wa daraja hilo utasaidia serikali kuongeza mapato katika mazao ya bishara na chakula.

“Barabara inaenda kuwakomboa wakulima wa wilaya ya Songea kwa kurahisisha huduma ya usafiri, na tunamshukuru sana Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Chama cha Mapinduzi kwa kusimamia vizuri ilani”

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Songea Vijijini Ndg. Thomas Masolwa amempongeza Mhe. Rais kwa kutatua changamoto kwa wananchi, na kwa kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Mto Njoka.

Awali katika taarifa wakala wa barabara vijijini TARURA Mhandisi Johnson Kweka alisema Mkandarasi HERA Construction ameshatekeleza kazi za kusafisha eneo la daraja, kuondoa miti katika eneo la mradi, kuchimba udongo na kupasua mawe kwa ajili ya ujenzi wa msingi wa daraja.

Amefafanua kwamba Mkandarasi anaendelea na ufungaji wa nondo na boksi kwa ajili ya ufungaji wa nguzo na mikono ya daraja na ujenzi umefika asilimia  40

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.