• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MIRADI ya BOOST na SEQUIP ilivyochochea maendeleo ya elimu Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: March 11th, 2025

Mkoa wa Ruvuma umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuboresha miundombinu ya elimu kupitia Programu ya BOOST, mradi mkubwa wa ujenzi wa shule mpya na ukarabati wa miundombinu ya shule za msingi.

 Jumla ya shule mpya za msingi 12 zimejengwa, pamoja na miundombinu mbalimbali katika shule za msingi 44, kwa gharama ya shilingi bilioni 7.29.

Ujenzi wa shule zote umefanikiwa kwa asilimia mia moja, na tayari shule hizo zimeanza kutumika, hatua inayotarajiwa kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wa mkoa huu.

Mbali na juhudi hizo, Mkoa wa Ruvuma pia umeendelea kupokea fedha kwa ajili ya miradi mingine muhimu ya elimu inayolenga kuinua viwango vya elimu ya sekondari kupitia Mradi wa Kuboresha Elimu ya Sekondari (SEQUIP).

Katika kipindi cha Januari 2021 hadi Desemba 2024, jumla ya shilingi bilioni 3.43 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 20, mabweni 22, na matundu ya vyoo 82.

Miradi hii inalenga kuboresha shule zilizopandishwa hadhi kuwa na madarasa ya kidato cha tano na sita, pamoja na shule zenye idadi kubwa ya wanafunzi, na inatekelezwa katika halmashauri za Namtumbo, Songea Vijijini, Songea Manispaa, na Tunduru.

Katika kuhakikisha walimu wanapata makazi bora, Mkoa wa Ruvuma umepewa shilingi milioni 950 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 10 za walimu, kila moja ikiwa na uwezo wa kuchukua familia mbili (2 in 1).

Ujenzi huu unatekelezwa katika halmashauri zote nane za mkoa, hatua inayotarajiwa kuboresha mazingira ya kazi kwa walimu na kuongeza ufanisi katika ufundishaji.

Mkoa pia umepokea zaidi ya shilingi bilioni 5 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya 9 za sekondari kupitia awamu ya tatu ya Mradi wa SEQUIP.

Shule hizi zitajengwa katika majimbo yote ya uchaguzi ndani ya Mkoa wa Ruvuma, ikiwa ni juhudi za kuimarisha upatikanaji wa elimu ya sekondari kwa vijana wa mkoa huu.

Miradi hii inadhihirisha dhamira ya serikali ya kuhakikisha kila mtoto anapata elimu bora kwa kuweka mazingira mazuri ya kujifunzia.

Mafanikio haya ni ushahidi wa uwekezaji wa serikali katika sekta ya elimu, hatua inayosaidia kujenga jamii iliyoelimika na yenye uwezo wa kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.