• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma kuanza biashara ya hewa ukaa

Imewekwa kuanzia tarehe: November 8th, 2023

Wilaya za Namtumbo na Tunduru mkoani Ruvuma zimeingia mkataba wa biashara ya hewa ukaa (Carbon) na Kampuni ya Tanzania Carbon(CT Limited) kutoka mkoani Arusha.

Mkataba wa kuanza biashara hiyo umesainiwa kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma mjini Songea chini ya Usimamizi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Ndugu Stephen Ndaki ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas.

Akizungumza kabla ya kusaini mkataba huo,Mkurugenzi wa Kampuni ya CT Limited Marc Backer amelitaja lengo la Kampuni ya Carbon Tanzania kuwa ni kuhakikisha wananchi  wanafaidika kiuchumi na  kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kupanda miti.

Amesema hapa nchini  wananchi wa vijiji nane katika Halmashauri ya wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi wameingiza zaidi ya bilioni 2.3 kwa kufanya biashara ya hewa ya ukaa.

“Mradi huu umewanufaisha wananchi wa wilaya za Tanganyika mkoani Katavi na Kiteto mkoani Manyara,hapa Ruvuma mradi wa biashara ya kaboni utakuwa mkubwa sana,tumeshapima tumegundua kuna kaboni nyingi sana’’,alisisitiza Backer.

Backer amesema biashara ya hewa ya ukaa ilianza rasmi mwaka 2018 katika Halmashauri ya Tanganyika mkoani Katavi kwa kuendeshwa na  Taasisi ya Carbon Tanzania ambapo mapato ya biashara hiyo yamekuwa yakipanda mwaka hadi mwaka.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Tunduru Wakili Julius Mtatiro  ameitaja mikataba ya biashara ya kaboni kuwa ina faida kubwa hata kama msitu utatunzwa kwa miaka 60 unaleta faida  kwa wananchi wenye misitu ikiwa ni Pamoja na kuleta mvua nyingi na kwamba wananchi watapata fedha nyingi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Mheshimiwa Ngollo Malenya amesema biashara ya hewa ukaa ni mradi mpya hapa nchini na kwamba baada ya majaribio katika wilaya ya Tanganyika serikali imeona faida kubwa.

Amesema biashara hiyo inamwezesha mwananchi kupata fedha baada ya kupanda miti ambapo ameitaja wilaya ya Namtumbo kuwa ni wilaya ya kimkakati kwa kuwa asilimia 19 ya maji yanayoingia kwenye mradi wa bwawa la Mwalimu Nyerere Rufiji yanatoka Namtumbo.

Amesisitiza kuwa biashara ya hewa ukaa ni mradi ambao utasaidia kutunza mazingira  na kuhakikisha kuwa uharibifu wa mazingira unakwisha na kwamba mradi utaleta mvua za kutosha na dhana ya Mkoa wa Ruvuma  kuwa ghala la Taifa la chakula itaendelea kuwepo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Ndugu Stephen Ndaki  amewaasa wakulima kuhakikisha wananufaika na mradi wa kaboni kwa kuhakikisha wanapanda miti ya kutosha badala ya kuishia kulima mahindi na mazao mengine.

Amewaasa wakulima kupanda miti kwa wingi na kuhifadhi misitu ili kupunguza hewa ya ukaa na kuongeza upatikanaji wa hewa safi lakini pia watakuwa wanafanya biashara ya hewa ya ukaa.

Tanzania imesaini  mikataba ya Kimataifa ambayo inahamasisha biashara ya hewa ya ukaa Duniani ambapo wananchi wanapopanda miti na kuhifadhi misitu inasaidia kufyonza na kupunguza hewa ya ukaa hewani  na kulipwa fedha hivyo kukuza uchumi wao.

Soko la hewa Safi ya Kaboni lililopo ni fursa muhimu kwani Dunia imedhamiria kuboresha Anga kutokana na madhara ya uharibifu wa hewa chafu ya kabon ili kuokoa anga na ongezeko la Joto duniani.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.