• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma na Morogoro kuunganishwa na barabara ya lami

Imewekwa kuanzia tarehe: January 23rd, 2023

SERIKALI kupitia Wakala za Barabara TANROADS inatarajia kuanza mradi wa kuunganisha Mkoa wa Ruvuma na Mkoa wa Morogoro kwa barabara ya lami.

 Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa nchini ambayo tayari wilaya zake zote zimeunganishwa kwa lami na makao makuu ya Mkoa.

Meneja wa TANROADS Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Ephatar Mlavi  amesema serikali inatarajia kutekeleza mradi wa ujenzi wa barabara ya Lumecha – Londo wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma hadi Kilosa – Kidatu mkoani Morogoro kwa kiwango cha lami.

Mhandisi Mlavi ameutaja mradi huo kuwa utahusisha ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami, yenye urefu wa kilometa 512 ambao ukikamilika utaunganisha Mkoa wa Ruvuma na Morogoro kwa kiwango cha lami

“Mradi huu upo katika hatua ya kupitia zabuni za wakandarasi ambapo zilifunguliwa tarehe 26 Agosti 2022. Mradi huu utatekelezwa kwa kutumia mtindo wa Usanifu, Manunuzi, Ujenzi na Ufadhili  (Engineering, Procurement, Construction and Financing”,alisema Mhandisi Mlavi.

Hata Hivyo Meneja huyo wa TANROADS Mkoa wa Ruvuma amesema utekelezaji wa mradi huo  unatarajia kuanza muda wowote baada ya hatua stahiki za manunuzi kukamilika.

Akizungumzia ujenzi wa Barabara ya Songea – Makambako kwa kiwango cha lami, Mhandisi Mlavi amesema serikali ya Awamu ya Sita inatarajia pia kutekeleza mradi wa ujenzi wa barabara ya lami sehemu ya Songea – Lutukira ikijumuisha na sehemu ya Mtwara korido yenye urefu wa kilometa 111.

Mhandisi Mlavi amesema katika utekelezaji wa mradi huo,Serikali tayari imeshaingia makubaliano na Mfadhili ambaye ni Benki ya Dunia na hivi sasa hatua za mradi huo zipo katika hatua za awali za manunuzi.

 Amebainisha Zaidi kuwa mradi huo utahusisha ujenzi wa kilometa 111 za lami ambazo zitajumuisha kilometa 14 za Songea bypass katika Manispaa ya Songea  na ujenzi wa barabara ya  Songea  hadi Lutukira Halmashauri ya Madaba yenye urefu wa kilometa 97 hivyo kuunganisha wilaya ya Songea mkoani Ruvuma na wilaya ya Njombe mkoani Njombe.

Hata hivyo amesema Mkoa wa Ruvuma kupitia Wilaya ya Nyasa tayari umeunganishwa na  Mkoa wa Njombe kupitia wilaya ya Ludewa kwa kutumia  daraja la mto Ruhuhu unaomwaga maji yake ziwa Nyasa.

Amesema mradi wa daraja la Ruhuhu ulianza  kutekelezwa Juni 2016 na kukamilika Oktoba 2021 kwa gharama ya Zaidi ya shilingi bilioni 8.9 ambao umeunganisha wilaya za Nyasa na Ludewa.

Katika mwaka wa fedha 2022/2023,TANROADS Mkoa wa Ruvuma iliomba bajeti ya Zaidi ya shilingi bilioni 41 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo. Hata hivyo, kiasi cha Zaidi ya Shilingi 28 ndiyo kimeidhinishwa kwenye bajeti ya 2022/2023.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Januari 23,2023

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.