• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma ulivyodhamiria kupunguza udumavu shule za bweni

Imewekwa kuanzia tarehe: September 19th, 2023

Afisa Elimu Mkoa wa Ruvuma Emmanuel Kisongo  amewataka wazabuni wanaosambaza vyakula katika shule za bweni kuleta chakula kilicho bora ili kusaidia kuondoa udumavu.

Kisongo amesema hayo wakati anazungumza katika kikao kazi cha kuboresha afua za afya na lishe katika shule za bweni Mkoa wa Ruvuma ambacho kilihudhuriwa na wadau mbalimbali na  kufanyika katika ukumbi wa sekondari ya Songea Girls.

Afisa Elimu huyo amesema kufanyika kwa kikao hicho  ni sehemu ya utekelezaji wa viashiria vya mkataba walishe unaozitaka shule zote kutumia vyakula vyenye viinilishe kwa wingi ili kuboresha lishe kwa vijana wa rika balehe.

“Tunatakiwa kupeana mbinu mbadala za kupata vyakula ambavyo vitasaidia kupunguza tatizo la udumavu, pia tunahimizwa matumizi ya vyakula vyenye virutubishi kama viazi lishe na mahindi lishe ulimaji wa bustani za mboga na matunda sambamba na matumizi ya mazao ya bustani’’,alisisitiza Kisongo.

Kwa upande wake Afisa Lishe Mkoa wa Ruvuma Neema Mtekwa amesema ni muhimu sana kuwekeza katika lishe hasa hizo siku 1000 za uhai wa mtoto, na kwamba kuna visababishi vya utapiamlo ambavyo ni ulishaji hafifu kwa watoto, vijana na makundi mengine maalumu.

 Kulingana na Afisa Lishe huyo, utafiti ulifanyika hivi karibuni umebaini kuwa angalau watoto wanaopewa chakula chenye mchanganyiko unao hitajika ni asilimia 20.6.

Naye,Mwakilishi wa   Afisa Ununuzi Mkoa wa Ruvuma  Anthony Luoga, amewaomba wazabuni wajitahidi kuleta chakula chenye ubora ili kusaidia kupunguza udumavu kwa watoto ambao wanaishi katika shule za bweni.

Mwezeshaji kwenye kikao hicho David Mwasanga  amewasisitiza elimu ya kilimo cha mahindi na mbogamboga  kwa wadau ili kuboresha lishe na kuondokana na udumavu kwa watoto.

Kikao kazi hicho kilishirikisha wataalam wa lishe,elimu,ununuzi,kilimo ,wazabuni,walimu wa chakula na wakuu wa shule za bweni

Imeandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Farida Mussa Baruti

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.