• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma una mbolea za kutosha msimu mzima

Imewekwa kuanzia tarehe: November 13th, 2020

MKURUGENZI Mtendaji  wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea nchini (TFRA) Dkt.Stephan Ngailo amesema Mkoa wa Ruvuma una mbolea  ya kutosha ya aina zote itakayokidhi mahitaji ya wakulima katika msimu mzima.

Akizungumza wakati anakagua ghala la mbolea la SONAMCU mjini Songea,Dkt.Ngailo amesema amekagua maghala ya mbolea katika wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma na ameridhika kuwa mbolea ipo ya kutosha.

Ametoa rai kwa wakulima kuendelea kujiandaa kununua mbegu na kulima mashamba yao ambapo amesema mbolea zote zipo za kutosha  ikiwemo urea,DP,SA na NPK.

Amesema serikali imekusudia kuhakikisha kuwa mbolea za aina zote zinapatikana katika mikoa inayolima mazao ya chakula ukiwemo Mkoa wa Ruvuma, Njombe, Iringa, Songwe, Rukwa, Katavi,Kigoma na Tabora na kwamba serikali imedhamiria kuhakikisha kuwa maeneo hayo yote yanapata mbolea ya kutosha.

“Katika nchi nzima tuna zaidi ya asilimia 60 ya mahitaji yote ya mbolea,tunatarajia kufikia kati ya mwezi Februari hadi Machi tutakuwa na asilimia 75 hadi 80 ya mahitaji yote ya mbolea nchini’’,amesisitiza Dkt.Ngailo.

Dkt.Ngailo amesema katika msimu huu,serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt.John Magufuli imejipanga vizuri kuhakikisha wakulima wanapata mbolea za aina zote kwa wakati.

 Hata hivyo amesema katika tathmini iliyofanyika Oktoba mwaka huu,Tanzania ilikuwa na tani zaidi ya 65,000 za mbolea ya urea na kwa mbolea nyingine zote zilifikia tani  252,000 ambapo kiasi hicho cha mbolea kinaweza kufika hadi mwezi Februri 2021.

Ameongeza kuwa hivi sasa katika bandari ya Dar es salaam kuna meli imetia nanga inaendelea kupakua mbolea aina ya urea tani 18,000 na kuna tani nyingine za mbolea zinatarajiwa kuingizwa nchini wakati wowote.

Kwa upande wake Afisa Kilimo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Paulo Msemwa  amesema mahitaji ya mbolea katika Mkoa ni tani zaidi ya 50,000 ambapo hadi sasa zimeingia tani zaidi ya 13,000 .Amesema mbolea imesambazwa katika maeneo yote ya Mkoa hivyo  ametoa rai kwa wakulima kuandaa mapema pembejeo zote za kilimo  ili kuongeza uzalishaji.

Mkoa wa Ruvuma  katika misimu miwili mfululizo ya 2018/2019 na 2019/2020 umeongoza na kushika nafasi ya kwanza kitaifa katika uzalishaji wa  mazao ya chakula,huku sababu kubwa ya kuongeza uzalishaji ni upatikanaji wa mbolea ya kutosha.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Novemba 13,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.