• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma unavyozalisha chakula na kutoa mchango mkubwa kiuchumi

Imewekwa kuanzia tarehe: August 10th, 2024

Na Albano Midelo

MKOA wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa michache maarufu nchini  inayozalisha chakula na kutoa mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa Taifa.

Hayo yamesema na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed wakati wa kufunga maonesho na sherehe za wakulima Nanenane ngazi ya Mkoa wa Ruvuma zilizofanyika katika viwanja vya Amanimakoro wilayani Mbinga.

Amesema chakula kinachozalishwa mkoani Ruvuma licha ya kutumika ndani ya Mkoa ,lakini pia kinatumika nje ya Mkoa na nje ya nchi hivyo kusaidia wananchi kupata kipato na kukuza uchumi.

Hata hivyo amewatahadharisha wananchi kutouza chakula chote badala yake wakumbuke kuweka akiba ya chakula ambacho kitawafikisha katika msimu mwingine wa mavuno.

“Serikali imeongeza bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kutoka Bilioni 275 hadi bilioni 295 mwaka huu,imeongeza pia bajeti ya Wizara ya Kilimo kutoka Zaidi ya shilingi bilioni 294 hadi kufikia shilingi Trilioni 1.3,hii yote ni dhamira thabiti ya Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ya kuinua sekta ya Kilimo,Uvuvi na Mifugo’’,alisema Kanali Abbas.

Katika hatua nyingine,Mkuu wa Mkoa ametoa maagizo mbalimbali kwa watendaji wa Halmashauri na Wilaya yakiwemo kusimamia matumizi sahihi ya vitendeakazi vilivyotolewa na serikali kwa maafisa Ugani,kuhakikisha uchaguzi wa viongozi wa serikali za mitaa unafanyika kwa utulivu na amani na kuhakikisha shule zenye maeneo yanayofaa wapande maharage lishe na miti ya matunda ili kusaidia wanafunzi kupata lishe.

Maagizo mengine ni Kamati za Pembejeo ngazi ya Wilaya zihakikishe zinakuwa na vituo vya kusambazia mbolea za ruzuku ya serikali na wataalam wa ufugaji Samaki waendelee kutoa elimu ya utengenezaji chakula cha Samaki na kuandaa mazingira wezeshi ya uwekezaji vyakula vya samaki.

Awali akizungumza kwenye maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Mheshimiwa Kisare Makori amesema Zaidi ya asilimia 85 ya wananchi wilayani Mbinga ni wakulima wa mazao ya chakula na biashara.

Makori  ameahidi kusimamia kilimo ili Wilaya hiyo iweze kutoa mchango mkubwa katika sekta ya kilimo na kuufanya Mkoa wa Ruvuma kuwa kinara katika uzalishaji wa mazao ya chakula  na wananchi waendelee kufaidika kupitia sekta ya kilimo.

Amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kulifanya eneo la Amanimakoro  kuwa endelevu katika maonesho ya Nanenane ya Mkoa kila mwaka ombi ambalo Mkuu wa Mkoa ameridhia.

Kaulimbiu ya mwaka huu ya maadhimisho ya sherehe za wakulima Nanenane ni Chagua viongozi bora wa serikali za mitaa kwa maendeleo endelevu ya kilimo,mifugo na uvuvi.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.