• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma wafikia asilimia 63 ya lengo la kuhesabu kaya 450.000

Imewekwa kuanzia tarehe: August 26th, 2022

Mkoa wa Ruvuma wafikia asilimia 63 ya lengo la kuhesabu kaya 450,000

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema takwimu ya kitaifa ya sensa inaonesha kuwa hadi kufikia Agosti 26 mwaka huu saa moja asubuhi Mkoa wa Ruvuma ulikuwa umefikia asilimia 63 ya lengo la Kuhesabu zaidi ya kaya 450,000.

Kanali Thomas amesema hayo wakati anazungumza na wananchi wa Peramiho nje kidogo ya Mji wa Songea alipofanya ziara ya kukagua zoezi la sensa linaloendelea nchini kote.

Amesema kutokana na takwimu hizo za kitaifa Mkoa unakwenda vizuri ambapo ametoa rai kwa wananchi kuendelea kushirikiana na makarani kwa kujitokeza kuhesabiwa ili Mkoa uweze kupata takwimu za sensa za watu za kutosha ambazo zitaisaidia serikali kupanga mipango ya maendeleo.

Hata hivyo Kanali Thomas amesema anatamani Mkoa wa Ruvuma uvunje rekodi za kitaifa kwenye majumuisho ya sensa kwa kuongoza kitaifa.

RC Thomas amewapongeza watendaji  kwa usimamizi mzuri katika zoezi la sensa  ambapo amewataka viongozi wa Halmashauri zote kuendelea  kuwaelimisha wananchi wajitokeze kuhesabiwa ili kufikia malengo ya Mkoa na taifa kwa ujumla

“Matumaini yangu tuakwenda vizuri  niwaombe wananchi wenzangu endeleeni kujitokeza ili tupate data sahihi, data hizi zina manufaa  kwetu na kwa taifa letu”alisema RC Thomas.

Naye Mkurugenzi wa Halmashaur ya Wilaya ya Songea Neema Maghembe ameeleza Halmashauri hiyo yenye Kata 16, inatarajia kuhesabu kaya  zaidi ya 36,000, na kwamba hadi kufikia Agosti, 25, wameweza kuhesabu kaya zaidi ya 28,000.

“Nikuhakikishie Mkuu wa Mkoa zoezi hili linakwenda vizuri na watu wanajitokeza kuhesabiwa, hata kaya uliotembelea umekuta zoezi linakwenda vizuri” alisema Bi maghembe.

Mkoa wa Mkoa wa Ruvuma, anaendelea na ziara ya kukagua maendeleo ya zoezi la sensa ya watu na makazi katika Halmashauri za Mkoa wa Ruvuma.Zoezi hili lilianza Agosti, 23, 2022 na linatarajiwa kukamilika Agosti, 28 mwaka huu.

Imeandikwa na Albano Midelo

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Agosti 26,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.