• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma wakusanya bilioni 21 kutokana na makaa ya mawe

Imewekwa kuanzia tarehe: November 16th, 2022

Mkoa wa Ruvuma umefanikiwa kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 21 kutokana na madini ya makaa ya mawe katika kipindi cha mwaka 2021/2022.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas wakati anatoa salama za Mkoa,kwenye mkutano wa wadau wa madini ya makaa ya mawe,uliofanyika kwenye ukumbi wa Parokia ya Bombambili mjini Songea.

Kanali Thomas amesema makusanyo hayo ni saw ana asilimia 179 ya lengo la mwaka,ambapo Mkoa ulipangiwa kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 12.

“Katika kipindi cha hivi karibuni,makaa ya mawe yamekuwa yanahitajika sana ulimwenguni kama chanzo cha nishati na hivyo kuwa moja ya chanzo kikubwa cha mapato ya serikali’’,alisisitiza.

Hata hivyo amesema katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2022/2023 Mkoa wa Ruvuma umepangiwa  kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 17 ambapo hadi kufikia Novemba 11,2022 tayari Mkoa umekusanya zaidi ya shilingi bilioni 15 sawa na asilimia 88.72.

Amesema hadi kufikia Juni 30,2023,Mkoa wa Ruvuma umelenga kukusanya mapato kutokana na madini ya makaa ya mawe yatakayofikia kati ya shilingi bilioni 35 hadi bilioni 40.

Naye Mgeni rasmi kwenye mkutano huo,Waziri wa Madini Dkt.Doto Biteko amewataka wawekezaji kwenye sekta ndogo ya makaa ya mawe kujenga mahusiano na jamii inayowazunguka.

“Wewe Mwekezaji uone aibu kuchimba makaa ya  mawe halafu watu Jirani ya mgodi wako  pale ni masikini wa kutupa,Watoto wao shuleni wanakaa chini,Mwekezaji unaingiza mapato ya bilioni mbili, lakini umeshindwa kujenga darasa la milioni 20 hiyo ni aibu’’,alisema Waziri Biteko.

Hata hivyo Waziri wa Madini amesema hivi sasa  ushirikishaji watanzania  katika sekta ya madini,serikali inafanya vizuri ambapo katika migodi yote nchini wafanyakazi waliopo,asilimia 97 ni  watanzania na katika migodi mingine asilimia 100 ni watanzania.

Amesisitiza kuwa katika hatua ya ushirikishwaji watanzania kwenye sekta ya madini,serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan inastahili kupongezwa kwa sababu zamani sekta hiyo ilimezwa kwa asilimia kubwa na wageni na kwamba zaidi ya asilimia 70 ya  bajeti yote ya manunuzi katika migodi mikubwa inanunuliwa na watanzania.

Mkutano wa wadau wa makaa ya mawe umefanyika mkoani Ruvuma ukishirikisha watendaji wote wa Wizara ya Madini na mikoa inayozalisha madini hayo ikiwemo Ruvuma, Njombe,Songwe na Mbeya.

Mkoa wa Ruvuma una hazina ya makaa ya mawe zaidi ya tani milioni 227 ambayo yanatarajiwa kuchimbwa kwa miaka 300.

Imeandikwa na Albano Midelo

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Novemba 16,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.