• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma wapokea mbegu bora za alizeti tani 52.712

Imewekwa kuanzia tarehe: November 30th, 2021

MKOA wa Ruvuma umepokea kilo Elfu 52,712 ya mbegu bora ya zao la Alizeti zenye thamani ya Sh.184,492,000 kutoka kwa wakala wa Mbegu Tanzania(ASA)ambazo zitauzwa kwa bei ya Sh.3,500 kwa kilo moja kwa wakulima wa  mkoa huo katika  msimu 2021/2022.

Hayo yamesemwa na Afisa Kilimo wa mkoa huo Onesmo Ngao,wakati akitoa taarifa ya kuwasili kwa mbegu hizo kwa mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge.

Ngao alisema, kawaida mbegu hizo uuzwa  kwa bei ya Sh.35,000 kwa kilo moja na wafanyabiashara, lakini serikali imeweka punguzo hadi kufikia Sh.3,500 kama jitihada za kuwawezesha  wakulima wengi waweze kununua na  kulima zao hilo.Alisema,mkoa wa Ruvuma umejipanga  kutekeleza kilimo cha mkataba ili kuunga mkono juhudi za Serikali ambapo  umepanga kulima hekta 9,291 ambazo zinatarajia kutoa mavuno ya tani 7,743 katika msimu wa kilimo 2021/2022.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge,amewaomba wakulima wa mkoa huo kupitia Halmashauri za wilaya kutumia fursa  hiyo kupata mbegu bora, kulima kwa tija na kuongeza uzalishaji wa zao hilo.

Alisema, ni matumaini ya Serikali ya mkoa na Taifa kuwa, mbegu hizo zitasaidia wakulima wengi kulima zao la Alizeti na hatimaye kufikia adhima ya Serikali kuwezesha upatikanaji wa mafuta ya kula ndani na nje ya mkoa.

Aidha Ibuge, amewataka kulima kwa kufuata maelekezo ya wataalam na kuwatumia maafisa ugani waliopo katika maeneo yao, na watoa huduma za pembejeo kulima kilimo cha kisasa badala ya kuendelea kulima kwa mazoea.

Ametoa wito kwa maafisa ugani kutimiza wajibu wao,na kuwahudumia wakulima ili mbegu hizo zilete tija katika uzalishaji na kuwanufaisha wakulima ambapo mkoa umejipanga kuhakikisha wanatumia mvua zilizoanza kunyesha kulima mazao mbalimbali ya chakula na biashara.

Alisema,lengo la Serikali ni kuleta tija na kuongeza upatikanaji wa mafuta ya kula ndani ya mkoa na nchi kwa ujumla, na kuipunguzia serikali gharama  ya kuagiza mafuta hayo nje ya nchi ndiyo maana imewekeza nguvu kubwa kuhakikisha uzalishaji wa zao hilo unaongezeka.

Ibuge ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan,kumsaidia mkulima kupata mbegu hizo kwa bei ya ruzuku kupitia wakala wa mbegu Tanzania(ASA)kwa kuwa zao hilo ni la kimkakati hali itakayowezesha watu wenye kipato cha chini kumudu bei.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.