• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma watekeleza agizo la Rais kujenga mahakama ya mwanzo Nakapanya

Imewekwa kuanzia tarehe: May 23rd, 2020

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amezindua jengo la mahakama ya mwanzo ya Nakapanya wilayani Tunduru lililogharimu zaidi ya shilingi milioni 55.

Ujenzi wa mahakama hiyo umetokana na agizo la Rais Dkt John Magufuli wakati wa ziara yake ya Aprili 4 mwaka jana aliposimama katika  tarafa ya Nakapanya kuwasalimia wananchi na kusikiliza kero zao.

Akizungumza kabla ya kuzindua jengo hilo,Mkuu wa Mkoa alisema wananchi hao walitoa kwa Rais, kero ya kufungwa kwa soko  kwa sababu ya kuwa  karibu na mahakama ndipo Rais Magufuli aliagiza litafutwe eneo jingine la kujenga mahakama hiyo.

“Katika kuunga mkono juhudi za ujenzi wa mahakama hii Rais alichangia shilingi milioni 10,tunamshukuru kwa moyo wake anavyojitolea kumaliza kero za wananchi wa Tanzania tukiwemo sisi wananchi wa Nakapanya’’,alisema Mndeme.

Mndeme amewaagiza TARURA kutengeneza barabara inayokwenda katika mahakama hiyo katika kiwango cha changarawe ili iweze kupitika mwaka mzima,pia amemwagiza Meneja wa TANESCO na RUWASA kupeleka umeme na maji katika jengo hilo.

 Naye Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro  amebainisha gharama zilizotumika katika ujenzi huo na wadau waliochangia hadi sasa kuwa ni Rais Dkt John Magufuli shilingi milioni 10,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma shilingi milioni 29,mfuko wa Jimbo milioni tatu na nguvu za wananchi zaidi ya milioni tatu.

Amesema mradi ulianza kutekelezwa Mei 2019 na ulitarajia kugharimu zaidi ya milioni 69 hadi kukamilika na kwamba kutokana na matumizi ya force account gharama halisi za ujenzi zimepungua na kufikia zaidi ya milioni 55.

“Jengo hili lina vyumba vinne vya ofisi,ukumbi mmoja,vyumba viwili vya mahabusu,choo cha ndani na vyoo viwili vya nje,mradi utasaidia kuboresha mazingira ya kazi kwa watumishi wa mahakama’’,alisisitiza Mtatiro.

Mtatiro amesema,mradi huo utawanufaisha kwa kupata haki za kisheria wananchi wa tarafa nzima ya Nakapanya yenye  kata za Nakapanya, Namakambale, Tinginya, Ngapa, Mindu, Namiungo, Majimaji na Muhuwesi.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa jengo hilo,Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Songea Jaji Isaya Alufan amempongeza Rais  kwa maamuzi ya busara kuamua kujenga mahakama  ya mwanzo Nakapanya ambapo amesema mahakama ni sehemu ya kutoa huduma kwa wananchi.

Hata hivyo amesema vitu vichache ambavyo ni maji,umeme na samani vikikamilika jengo hilo litaanza kutoa huduma kwa wananchi ,ameahidi Idara ya Mahakama ipo tayari kushirikiana na serikali kuhakikisha kuwa mapungufu yanafanyiwa kazi haraka ikiwemo kuwaleta watumishi wa mahakama na samani ili kazi ianze.

Kukamilika kwa mahakama ya mwanzo Nakapanya kunaifanya wilaya ya Tunduru kuwa na mahakama za mwanzo  saba.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Mei 23,2020

Tunduru

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.