• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma watoa chanjo ya polio kwa asilimia 122

Imewekwa kuanzia tarehe: May 19th, 2022

MKOA wa Ruvuma umefanikiwa kutoa chanjo ya polio kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano kwa asilimia 122 .

Akizungumza kwenye kikao cha Mkoa cha  utekelezaji wa kampeni ya utoaji wa huduma za chanjo ya polio kilichofanyika mjini Songea,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amesema Mkoa umepata mafanikio makubwa katika awamu ya kwanza ya utoaji chanjo ya polio.

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mheshimiwa Pololet Mgema,amesema katika awamu ya kwanza ya utoaji chanjo ya polio,Mkoa ulipanga kuchanja watoto 241,966 ambapo waliochanjwa walikuwa ni watoto 293,543 sawa na asilimia 122.

‘’Mkoa wa Ruvuma umekuwa kinara katika utoaji chanjo ya polio kati ya mikoa minne ya awamu ya kwanza iliyotekeleza kampeni,pia Mkoa wa Ruvuma ulikuwa kinara kwa utaoji chanjo za kawaida mwaka 2021’’.alisisitiza RC Ibuge.

Kwa mujibu wa RC Ibuge, katika chanjo ya UVIKO 19 ambayo Mkoa ulianza kuchanja Agosti 2022,Mkoa umechanja jumla ya watu 409,323 kati yao watu 322,363 sawa na asilimia 78.76 wamekamilisha dozi na watu 86,960 wamepata dozi ya kwanza.

Hata hivyo amesema ili kufikia asilimia 70 ya uchanjaji Mkoa wa Ruvuma,unatakiwa kuchanja watu 670,557 ambao ni asilimia 70 ya watu 957,938 wenye umri wa Zaidi ya miaka 18 ambao ndiyo wenye sifa ya kupatiwa chanjo ya UVIKO.

Amesema hadi kufikia Mei 15 mwaka huu,Mkoa wa Ruvuma umechanja watu 322,363 ambao wamekamilisha dozi sawa na asilimia 48.07 ya watu 670,557.

Kwa upande wake Mratibu wa chanjo Mkoa wa Ruvuma Winbroad Mvile amelitaja lengo la kampeni  za utoaji huduma za chanjo ya polio ya matone kwa watoto chini ya miaka mitano ni kuzuia uwekezekano wa watoto kupata madhara yatokanayo na virusi vya polio.

Hadi sasa visa viwili vya polio vimegundulika katika nchi mbili jirani  na Mkoa wa Ruvuma za Malawi na Msumbiji hivyo chanjo inasaidia kuzuia mlipuko wa ugonjwa huo kwa watoto baada ya kupata chanjo.

Imeandikwa na Albano Midelo

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Mei 19,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.