• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa majeshi awataka wananchi kuwaenzi mashujaa

Imewekwa kuanzia tarehe: February 27th, 2025

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob John Mkunda, amewataka wananchi kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuokoa Taifa dhidi ya maadui ujinga, maradhi na umasikini, pamoja na kuwaenzi mashujaa waliopigana na kufa kwa ajili ya Taifa.

Ametoa rai hiyo wakati akisoma hotuba kwenye maadhimisho ya kumbukumbu ya mashujaa wa Vita vya Majimaji, ambapo alikuwa mgeni rasmi wa maadhimisho hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Songea 

"Rai yangu ni kwamba mashujaa waliolala mahali hapa na kwingineko watutie hamasa kupambana kadri tuwezavyo ili kuokoa Taifa letu dhidi ya maadui hao, maana bado wapo. Kuendekeza uvivu, uzembe, madawa ya kulevya, rushwa, ubadhilifu wa mali za umma na malalamiko bila kufanya kazi ni kuzisaliti roho zilizoangamizwa na wakoloni kwa ajili yetu," alisema Jenerali Mkunda.

Pamoja na mambo mengine, Jenerali Mkunda amesema mashujaa hao waliangamia kuulinda utamaduni wa Mtanzania, na hivi sasa vilio ni vingi vya mmonyoko wa maadili ya kitanzania, hali inaonyesha kuwa msimamo wa mashujaa umeachwa, hivyo ni wakati wa kujitathmini na kuwaenzi mashujaa kwa kuuenzi utamaduni uliolindwa na mashujaa kwani ndio unaotambulisha Taifa la Tanzania.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amesema maadhimisho hayo, ambayo yamekuwa yakiratibiwa na Ofisi ya Mkoa, Wizara ya Maliasili na Utalii, na Baraza la Mila na Desturi la mkoa, licha ya kuwakumbuka mashujaa, kwa mwaka huu Wizara husika imeamua kutumia maadhimisho hayo kuhamasisha utalii wa utamaduni na malikale ili kujiletea maendeleo na kutia chachu ya maadhimisho hayo.

Kanali Ahmed ameongeza kuwa, kupitia maadhimisho hayo, Mkoa umeendelea kupata fursa za kiuchumi kupitia wageni mbalimbali waliokuja kwa ajili ya maadhimisho hayo na kutembelea vivutio vilivyopo mkoani hapo.

Kwa upande wake, Chifu wa Wangoni, Emmanuel Zulu, amesema wamekuwa wakiziheshimu sana kumbukumbu hizo na zina machungu mengi kutokana na kile walichotendewa mashujaa wa Vita vya Majimaji.

Kilele cha maadhimisho ya kumbukizi  ya mashujaa wa Vita vya Majimaji hufanyika Februari 27 kila mwaka, ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni "Makumbusho ya Majimaji na Malikale Zetu kwa Maendeleo ya Utalii na Uchumi."

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.